Sunday 29 October 2017

Samatta afikisha mechi 69 akiwa na KRC Genk jana

Samatta afikisha mechi 69 akiwa na KRC Genk jana

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta jana amecheza mechi yake ya 69, timu yake, KRC Genk ikilazimisha sare ya 0-0 na wenyeji, KV Kortrijk katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza A, Ubelgiji uliofanyika Uwanja wa Guldensporen mjini Kortrijk.

Samatta alicheza kwa dakika 70 kabla ya kumpisha  Nikolaos Karelis aliyekuwa anarejea uwanjani kwa mara ya kwanza baada ya kuwa nje kwa muda mrefu kutokana na kuwa majeruhi.

Katika mechi hizo 69, Samatta, mshambuliaji wa zamani wa Mbagala Market, African Lyon na Simba za Tanzania, amefunga mabao 22 kwenye mechi za mashindano yote tangu alipowasili Genk Januari mwaka jana akitokea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Katika mechi hizo, Samatta ambaye ni mshindi wa tuzo ya Mwanasoka Bora Anayecheza Afrika mwaka jana alipokuwa na Mazembe, 41 ameanza na mechi 24 ametokea benchi.

Kikosi cha KV Kortrijk kilikuwa: Kaminski, Verboom, Kovacevic, Rougeaux, Attal, D'Haene/Kagé dk84, Vanderbruggen, Azouni, Ajagun, Chevalier and Perbet/Budkivskyi dk72.

KRC Genk : Vukovic, Uronen, Colley, Aidoo, Mata/Maehle dk74, Heynen, Writers, Malinovskyi/Buffalo dk87, Pozuelo, Samatta/Karelis dk70 na Ingvartsen.

No comments:

Post a Comment