Tuesday 31 October 2017

Yanga kumkosa Juma Abdul kwenye mechi dhidi ya Singida United

Yanga kumkosa Juma Abdul kwenye mechi dhidi ya Singida United



Wakati Yanga itakuwa na kibarua cha kuivaa Singida United kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida, wikiendi hii, taarifa za uhakika zinaeleza, itamkosa beki wake wa kulia, Juma Abdul.

Abdul ana kadi tatu za njano, ya mwisho akiwa ameipata katika mechi dhidi ya Simba, Jumamosi.

"Juma ana kadi tatu, kadi ya tatu ameipata dhidi ya simba baada ya kupata nyingine dhidi ya Kagera. Hivyo hatacheza mechi ya Singida," taarifa zilieleza.

Hakuna mtu wa benchi la ufundi la Yanga alipatikana kuzungumzia baada ya simu zao kuwa zinaita bila majibu.

Lakini taarifa nyingine zikaeleza kuwa, tayari Yanga wana taarifa kuhusiana na Juma Abdul.

"Hatakuwa katika mipango ya safari, benchi la ufundi linajua Juma ana kadi tatu.

No comments:

Post a Comment