Friday 3 November 2017

Wahukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kumbaka mpwa wao



Mahakama moja nchini India imewahukumu watu wawili kifungo cha maisha jela kwa kumbaka mpwa wao mwenye umri wa miaka 10 ambaye alijifungua mtoto wa kike mnamo mwezi Agosti.

Wanaume wote wawili walikuwa wajomba wa smichana huyo.

Walihukumiwa kwa kumbaka msichana huyo siku ya Jumanne.

Uja uzito wa msichana huo ulibainika katikati ya mwezi Julai wakati alipopelekwa hospitalini baada ya kulalamikia maumivu ya tumboni.

Mjombake wa pili alikamatwa baada ya chembechembe za DNA za mtoto huyo kutofanana na kakake mkubwa ambaye ndio mshukiwa wa kwanza .

Kesi ya mshukiwa wa kwanza ilichukua mwezi mmoja huku mjombake mdogo akihukumiwa baada ya kesi hiyo kuchukua siku 18.

Kesi hiyo ya msichana wa miaka 10 imegonga vichwa vya habari kwa wiki kadhaa nchini India na kote duniani.

Alikuwa na uja uzito wa wiki 30 wakati mahakama moja ya Chandigarh ilipokataa ombi la kuavya mimba, kwa sababumimba hiyo ilikuwa kubwa.

Jopo la madaktari lilisema kuwa kutolewa kwa mimba hiyo ni hatari .

Baadaye mahakama ya juu ya India pia ilikataa kutolewa kwa mimba hiyo kwa sababu kama hizo za kimatibabu.

Sheria ya India hairuhusu kutolewa kwa mimba baada ya wiki 20 hadi pale daktari aweze kubaini kwamba maisha ya mama yapo hatarini.

Mtoto huyo hakujua kwamba alikuwa akibeba uja uzito na kwamba alielezewa kwamba tumbo lake likuwa na jiwe, kulingana na mwamndishi wa BBC Geeta Panday mjini Delhi.

Alijifungua mwezi Agosti na mtoto huyo kukabidhiwa mamlaka ya kuangalia watoto ili kulewa.

Awali msichana huyo aliwaambia maafisa wa polisi na wanaharakati wa maslahi ya watoto kwamba alibakwa mara kadhaa katika kipindi cha miezi saba iliopita na mjombake mkubwa ambaye yuko katika umri wake wa 40

No comments:

Post a Comment