Tuesday 31 October 2017

Korea Kaskazini: Watu zaidi ya 200 wafariki katika ajali baada ya majaribio

Watu zaidi ya 200 waripotiwa kufariki baada ya handaki moja  kuporomoka nchini Korea Kaskazini

Watu zaidi ya 200 waripotiwa kufariki na wengine kadhaa kukwama baada ya handaki moja likiwa katika ujenzi kuporomoka.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na runinga ya Japan, handaki moja katika ujenzi limeporomoka katika eneo ambalo limetaarishwa kawa ajili ya majaribio la makombora ya nyuklia Punggye-ri.

Taarifa zinafahamisha kuwa watu takriban 200 wamefariki baada ya kuporomoka kwa handaki hilo baada ya jaribio la kombora la nyuklia Korea Kaskazini.

Ajali hiyo  imethibitishwa pia na kituo cha habari cha Korea Kusini Yonhap.

Maporomoko mengine yametokea wakati shughuli za uokozi zikiendele

No comments:

Post a Comment