Thursday 2 November 2017

Mwanamuziki huyu afariki Dunia

Mwanamuziki Keith Wilder(65) amefariki dunia. Wider alikuwa akifanya vizuri na bendi yake ya Heatwave  kipindi cha miaka ya 70.

Kupitia bendi yake hiyo wameshafanya hits song kama “Always and Forever,” “Boogie Nights” na “The Groove Line”, chanzo cha kifo chake kimetajwa kuwa ni matatizo ya kiafya.

Taarifa ya kifo cha mkongwe huyo wa burudani imetolewa na binamu yake Billy Jones, ambaye ameeleza kuwa siku ya Jumapili marehemu alikuwa amelala na ndipo kifo kilipomkuta.

Kupitia band yake wameshawahi kushiriki tuzo kubwa duniani za Grammys mara mbili ila hawakuwahi kushinda tuzo hizo.


No comments:

Post a Comment