Monday 22 January 2018

Ronaldo apasuliwa uso



LICHA ya ushindi wa bao 7-1 dhidi ya Derpotivo la Coruna walioupata Real Madrid katika La Liga, mshambuliaji wake, wa Kimataifa Raia wa Ureno, Cristiano Ronaldo alikutana na dhoruba baada ya kuumia kwa kupasuka usoni.

Ronaldo aliumia kwa kuchanipa sehemu ya usoni baada ya kugongwa wakati akijaribu kufunga.

Alikuwa ameruka kichwa kwa lengo la kufunga lakini akagongana na mchezaji wa Derpotivo. Hata hivyo, Ronaldo alipata huduma nzuri na kilichovutia zaidi ni yeye kutumia simu ya daktari kuangalia kama alikuwa ameumia au la.

No comments:

Post a Comment