Friday 26 January 2018

Nyumba za Askari Magereza zatakiwa kukamilika ndani ya miezi mitano


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali mstaafu, Projest Rwegasira ametoa miezi mitano kwa Wakala wa Majengo (TBA) kukamilisha ujenzi wa nyumba za askari wa Jeshi la Magereza zilizoko Ukonga jijini Dar es Salaam.

Ametoa agizo hilo leo Ijumaa Januari 26,2018 alipofanya mazungumzi na maofisa wa TBA na wa Jeshi la Magereza baada ya kukagua ujenzi huo.

“…fanyeni juu chini mhakikishe mradi huu unakamilika ndani ya miezi hiyo mitano mliyosema. Ongezeni nguvu ili mkamilishe mradi huu kwa wakati,” amesema katika taarifa iliyotolewa na wizara.

Fedha za ujenzi wa nyumba hizo unaogharimu  Sh10 bilioni zilitolewa na Rais John Magufuli baada ya kufanya ziara Ukonga mwishoni mwa mwaka 2016.

Soma: Waziri Mkuu aagiza wakala wa majengo Mara kukamatwa

Ujenzi ulianza mwaka jana badala ya Desemba 19, 2016.

No comments:

Post a Comment