Saturday 27 January 2018

Wakimbizi kutoka Kongo wazidi kumiminika nchini


Zaidi ya raia 800 kutoka jamhuri ya kidemikrasi ya Kongo wamewasili mjini kigoma kuomba hifadhi ya ukimbizi nchini wakidai kukimbia vita katika nchi hiyo.

Raia hao wa DRC ambao wengi ni wanawake na watoto wametokea mashariki ya nchi hiyo na wamewasili kwa maboti kwa nyakati tofauti katika bandari ndogo ya Kibirizi mjini kigoma na kueleza kuwa hali ya vita katika nchi hiyo ni mbaya na kuomba serikali ya Tanzania kuwapokea.

Mkuu wa mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga akiambatana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa amefika katika eneo hilo na kueleza kuwa wamewapokea lakini serikali inafanya tathmini ya ujio wao.

No comments:

Post a Comment