Friday 26 January 2018

Wenger ajigamba kuhusu usajili wake


Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amesema timu hiyo haitauza mchezaji bila kununua mchezaji huku pia akiongelea usajili wa Aubameyang kuwa bado haujakamilika.

Kocha huyo mkongwe ameyasema hayo leo alipokuwa akitoa ripoti ya majeruhi na programu za timu kwa ujumla, ambapo amesisitiza nyota wake Olivier Giroud hauzwi kama ambavyo imekuwa ikiripotiwa.

''Kwasasa hauzwi mchezaji yoyote bila kununua mchezaji wa kuchukua nafasi yake, tumemuuza Sanchez lakini tumempata Mkhitaryan hivyo timu iko vizuri na kikosi cha wachezaji waliopo'', amesema Wenger.

Pia Mfaransa huyo ameongeza kuwa milango pekeee itakayokuwa wazi ni kwa timu za vijana ambapo kuna baadhi watatolewa kwa mkopo na wengine watapandishwa kwenye kikosi cha wakubwa.

Kuhusu kumsajili nyota wa Gabon na Borussia Dortmund Pierre Aubameyang, Wenger amesema bado hawezi kusemea lolote kwasababu hakuna kilichokamilika na mchezaji huyo bado ni mali ya Dortmund.



No comments:

Post a Comment