Friday 26 January 2018

Wanaovamia Maeneo Ya Serikali Kukiona Cha Moto Dar


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amewataka wananchi wanaopenda kuvamia maeneo ya Serikali yakiwemo maeneo ya shule kuacha na kuondoka mara moja kwani hatua Kali za kisheria  dhidi yao zitachukuliwa ikiwa pamoja na kufikishwa mahakamani.

Makonda amesema hayo leo jijini Dar es Salaam, alipokuwa anazindua uezekaji paa wa Ofisi za Walimu katika shule ya Msingi Mapinduzi iliyopo katika manispaa ya Kinondoni  na kusema kuwa kutokana na shule kutokuwa na uzio watu  wamekuwa wakijiamulia kujenga au kufanya makazi katika maeneo ya shule kitendo ambacho si sahihi.

"Wale wanaojipangia kuhamia au kuvamia maeneo yaaliyo wazi ya Serikali yakiwemo maeneo ya shule, hospitali na mengineyo  na kufanya makazi  kuacha mara moja tabia hiyo kwani kwa kufanya hivyo hatua Kali za kisheria zitachukuliwa ikiwemo kufikishwa mahakamani".Amesema Makonda.

Amesema watu wakihamia na kujenga maeneo ya shule watoto wao watasomea wapi hivyo tujiulize  kuvamia maeneo ya shule na kujenga ni kosa na wanaofanya hivi wachukuliwe hatua na kufikishwa mahakamani kwa yeyote atakaye uza au kununua maeneo hayo.
Aidha amesema wanaboresha mazingira ya kazi kwa walimu ikiwa ni kuendelea kusupoti kauli ya Rais Magufuli ya Mpango wa Elimu bure bila malipo wameamua kuboresha mazingira ya kazi kwa Walimu katika Mkoa huo kwa kujenga ofisi zipatazo 402,ambapo Leo Amezindu uzwkaji Paa katika ofisi hizo katika shule hiyo manispaa ya Kinondoni.

"Lazima mpishi awe anapika vizuri ili walaji waweze kula ivyo tunaboresha mazingira ya walimu wetu ili waweze kufanya kazi kwa uledi na ufanisi mkubwa ili watoto wetu waweze kufaulu vyema"Amesema

Kwa  upande Meya wa Mnispaa ya Kinondoni Mhe.Benjamani  Sitta memshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuangalia suala la Ofisi pamoja na nyumba za kwa Mkoa huo kwani ilikuwa ni changamoto kubwa sana kwa walimu walikuwa hawana ofisi kitendo kinachopelekea walimu kukaa chini ya miti na kufanya kazi zao.




No comments:

Post a Comment