Saturday 27 January 2018

Watu 30 Wapoteza Maisha Katika ajali ya moto Korea Kusini

Imethibitika zaidi ya watu 30 wamekufa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika ajali ya moto uliotokea katika Hospitali moja nchini Korea Kusini.

Hata hivyo maafisa wa nchi hiyo wanasema idadi ya waliokufa huenda ikaongezeka kutokana na baadhi ya watu kujeruhiwa vibaya.

Imefahamika kuwa moto huo ulianzia katika chumba cha dharura cha Hospitali ya Sejong, kusini mashariki mwa nchi hiyo.

Zaidi ya majeruhi 100 wanasemekana wamo katika jengo la hospitali hiyo.

Mwaka jana watu 29 walikufa katika mji wa Echeon, Korea Kusini, na wengine kujeruhiwa baada ya moto kuzuka katika sehemu ya mazoezi ya wazi.

No comments:

Post a Comment