Thursday 25 January 2018

Waziri Kigwangalla atoa agizo kwa Jeshi la Polisi


Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamisi Kigwangalla amesema anawajua vigogo wanne waliopanga mauaji ya muhamasishaji wa utalii ‘Wayne Lotter’ mwaka jana na kulitaka jeshi la polisi liwakamate watu hao ingawaje hajawataja hadharani.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo mjini Dodoma, Dkt. Kigwangalla amelitaka jeshi hilo lichukue hatua haraka za kuwakamata vigogo hao la sivyo ataenda moja kwa moja kutoa taarifa kwa Amiri jeshi Mkuu.

“Nawajua watu 4 waliopanga mauaji ya mhamasishaji wa utalii Wayne Lotter, watu hao ni vigogo na wanajulikana,“amesema Dkt. Kigwangalla.

Waziri Kigwangalla amesema ndani ya kipindi cha siku 100, Wizara yake imebaini mitandao 74 ya watu wanaojihusisha na ujangili ikiwa na washiriki 949 ambapo amedai baadhi ya washiriki hao tayari wameshafikisha Mahakamani kujibu tuhuma hizo.

Kuhusu kifo cha Mwanaharakati Wayne Lotter soma zaidi kwa kubonyeza link hii “Mwili wa mwanaharakati wa tembo aliyeuawa kwa risasi kuagwa Dar“.

No comments:

Post a Comment