Monday 22 January 2018

Wazazi wanashikiliwa na Polisi kwa kupokea mahali ya Ng'ombe saba


JESHI la Polisi mkoani Geita linawashikilia watu  wawili wakazi wa  Kijiji cha Kasubuya  wilayani Nyang’wale kwa kula njama wakiwa wazazi  kupokea mahari ya ng’ombe saba na kumwozesha  mwanafunzi wa  kidato cha pili.

Binti huyo  aliyekuwa anasoma katika shule ya sekondari Nyijundu, sasa ana ujauzito.

Aliyethibitisha kukamatwa kwa wazazi hao wa pande zote mbili ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita, Mponjoli Lotson na kuwataja ni baba mzazi wa msichana huyo, Herman Makanika (48) na Maximillian Makila ambaye ni baba mzazi wa mtuhumiwa aliyemuoa mwanafunzi huyo.

Ingawa hakulitaja jina la mtuhumiwa, Kamanda Mpojoli alimpongeza mwalimu wa shule ya sekondari aliyetoa taarifa  za kuwapo kwa tukio hilo na akabainisha  jinsi wazazi wa pande zote mbili walivyoshiriki  kutenda kosa licha ya mtuhumiwa kutoroka.

Alisema wazazi wa pande zote mbili wanahusika ingawa mtuhumiwa (muoaji) anaendelea kusakwa, hivyo wanapaswa kuwajibika kutokana na kufanya makubaliano kwa kutoa mahari ya ng’ombe saba na mzazi wa msichana kuwapokea ng’ombe hao kama mahari.

Aliongeza kuwa baada ya polisi kuarifiwa ilichukua hatua za haraka na watuhumiwa kukamawta na hadi jana walikuwa wanaendelea kushikiliwa huku juhudi za kumsaka mtuhumiwa zikiendelea kuhakikisha anapatikana na kuwajibishwa kwa mujibu wa sheria.

No comments:

Post a Comment