Thursday 19 October 2017

Nyalandu Akomalia katiba

Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM) amefunguka na kusema katika kikao cha Tisa cha Bunge kinachotarajiwa kuanza Novemba 7, 2017 Dodoma anakusudia kuwasilisha azma yake ya kupeleka muswada binafsi utakao weka sharti la kurejea mjadala wa Katiba Mpya.
Nyalandu amesema hayo leo kupitia mitandao yake ya kijamii na kusema amekusudia kufikisha jambo hilo mbele ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai.
"Nakusudia kuwasilisha kwa spika wa Bunge Mh. Job Ndugai. Azma yangu ya kuleta muswada binafsi wa sheria katika kikao kijacho cha Bunge itakayoweka sharti la kurejea upya mjadala wa Katiba Mpya ya Tanzania, kwa kuzingatia rasimu ya Katiba kama ilivyowasilishwa na Tume ya Jaji Warioba" alisema Lazaro Nyalandu
Suala la Katiba Mpya licha ya kuwa siyo kipaumbele cha Rais John Pombe Magufuli lakini wadau mbalimbali wamekuwa wakilizungumzia wakisema kuna haja kubwa ya mchakato huo wa Katiba mpya kuendelea sasa wakidai kuwa huu ni wakati sahihi zaidi mchakato wa Katiba Mpya kuendele

No comments:

Post a Comment