Sunday 15 October 2017

Larry Flynt atangaza zawadi ya dola milioni 10 kumuondoa Trump Madarakani

Mchapishaji wa jarida la picha chafu za utundu, Larry Flynt, amechapisha tangazo katika gazeti la Washington Post, akiahidi kulipa zawadi ya dola milioni 10, kwa mtu mwenye habari, zitazopelekea Rais Trump kushtakiwa na kuondoshwa madarakani.
Bwana Flynt, anayemiliki jarida la "Hustler", amesema ni wajibu wa kila Mmarekani, kumuondoa Bwana Trump, kabla ya kuchelewa.
Tangazo hilo, linatoa nambari ya simu ya kupiga na anuani ya barua pepe.
Larry Flynt, ambaye alikuwa mfuasi mkubwa wa Hillary Clinton katika kuania urais, ametoa matangazo kama hayo kabla, lakini hakuwahi kutoa zawadi kubwa kama hiyo.

No comments:

Post a Comment