Sunday 15 October 2017

MICHEZO: Ibrahim Ajib Azidi kumpoteza Niyonzima,,,,,,

Haruna Niyonzima na Ibrahim Ajib ni wachezaji waliozungumzwa sana wakati wa dirisha la usajili kabla ya kuanza kwa msimu huu kwa sababu ya kuhama kutoka klabu zao na kujiunga na mahasimu wa klabu walizozihama. Ajib kutoka Simba kwenda Yanga Niyonzima kutoka Yanga kwenda Simba.
Inatajwa kwamba Ajib alisajiliwa na Yanga kwa Tsh. 50 Mil pamoja na gari ndogo ya kutembelea (Toyota Brevis). Wakati huo ikielezwa Niyonzima ndiye mchezaji ghali kusajiliwa msimu huu baada ya kuvuta mtonyo unaokadiriwa kufika Tsh. 120 Mil.
Baada ya ligi kuanza Ajib ameshafunga magoli matatu na ku-assist moja katika mechi sita alizocheza huku Yanga ikiwa imefunga magoli sita kwenye ligi wakati Niyonzima bado hajafunga wala kutoa assist katika magoli 14 ambayo Simba imefunga hadi sasa, amecheza mechi nne kati ya tano.
Ibrahim Ajib
Njombe Mji 0-1 Yanga (Ajib)
Yanga 1-0 Ndanda (Ajib)
Kagera Sugar 1-2 Yanga (Ajib-assist goli la kwanza likafungwa na Chirwa, yeye akafunga la pili).
Haruna Niyonzima
Simba 7-0 Ruvu Shooting (hakufunga wala ku-assist)
Azam 0-0 Simba
Mbao 2-2 Simba (hakufunga wala kutoa assist)
Stand United 1-2 Simba (hakufunga wala ku-assist)
Ligi bado inaendelea bado kuna fursa ya kuona mambo mengi kutoka kwa mafundi hawa wawili ndani ya ligi yetu, Niyonzima anaweza akanyanyuka na kumfikia Ajib hata kumwacha lakini pia inawezekana Ajib akaendelea kumkimbiza Niyonzima kama ilivyo sasa hivi.

No comments:

Post a Comment