Monday 16 October 2017

Zitto amkumkumbuka Mh. Filikunjombe ‘Ni majaribu makubwa kukubali kuwa haupo nasi’

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amemkumbuka marehemu Mbunge wa jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe ambae alifariki dunia baada ya helikopta aliyokuwa akiitumia kwaajili ya kampeni kupata ajali kwenye msitu wa Selous.
Mbunge Zitto amesema kuwa Filikunjombe alikuwa rafiki yake na ndugu yake hivyo bila uwepo wake ni majaribu makubwa.
Rafiki yangu, Ndugu yangu. Miaka miwili Sasa bila kuwa nawe. Ni majaribu makubwa kukubali kuwa haupo nasi. Mola akuweke mahala peponi. Naendelea kuombea familia moyo wa subira.
Ninakukumbuka Ndugu yangu Deo Haule Filikunjombe
Mhe. Deo Filikunjombe na abiria wengine walikuwa kwenye helikopta yenye namba 5Y-DKK wakitokea Dar kuelekea Ludewa.

No comments:

Post a Comment