Sunday 15 October 2017

Burudani : Nuh Mziwanda Afunguka maumivu anayoyapata,,,,,

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Nuh Mziwanda ambaye hivi karibuni ameachana na mke wake, amesema kuwa kitendo hicho kinamuumiza sana kwani anakosa muda wa kuwa na mtoto wake, na anahisi mtoto wake atakuwa bila kupata malezi yake.
Kwenye ukurasa wake wa instagram Nuh Mziwanda ameandika ujumbe akionyeshwa kuumizwa na kuwa mbali na mtoto wake huku akilelewa na watu wengine, wakati yeye baba yake yupo, lakini anashindwa kutimiza wajibu wake wa kumlea kutokana na ugomvi uliopo kati yake na mama mtoto wake ambaye wameshaachana, huku akijtahidi
"Nakumiss sana Mwanangu Anya, yani Mungu anajua jinsi gani Moyo wangu unaenda mbio nikikukumbuka au ukinijia akilini, maana najua haufurahi, najua hauhisi upendo kama uliokua unahisi kipindi upo karibu yangu, napenda ningekukuza kwenye misingi yangu, sheria zangu na kanuni zangu kama baba yako, ukweli nipo kwenye wakati mgumu sana sana kwa ajili yako wewe tu, najitatahidi kucheka ila ukweli naumia na majonzi mengi juu yako", ameandika Nuh Mziwanda.
Nuh Mziwanda ameendelea kuandika ujumbe huo akisema anamwachia Mungu kwa yote yanayotokea, huku akimlaumu mama mtoto wake kwa malezi ambayo anampa, kwani sio yale anayostahili mtoto wa umri wake kuyapata.

No comments:

Post a Comment