Sunday 21 January 2018

Jafari Maganga: Watanzania wameanza kukubali falsafa ya Azam FC


Kuelekea mchezo wa leo wa ligi kuu soka Tanzania Bara kati ya Tanzania Prisons dhidi ya Azam FC, msemaji wa wa Azam FC Jafar Idd Maganga amesema watanzania wameanza kukubali falsafa ya timu hiyo ya kutumia vijana.

Jaffar amesema kocha mkuu wa timu hiyo Aristica Cioaba, amekuwa muumini wa kutumia vijana kitu ambacho awali kilionekana kupingwa na mashabiki wengi wa soka wakiamini kuwa timu hiyo haitafanya vizuri.

''Watanzania wengi wameshaanza kukubali na wanaunga mkono uongozi wa Azam FC kuwatumia vijana na kocha huyu (Cioaba) amekuwa akiwaamini zaidi vijana tofauti na makocha wetu waliopita'', amesema Jaffar.

Kuhusu mchezo wa leo jioni, Jaffar amesema benchi la ufundi limejipanga kuhakikisha linapanga wachezaji ambao wataendana na timu ya Tanzania Prisons pamoja na hali ya uwanja wa Sokoine ili kuhakikisha timu yao inapata matokeo mazuri.

Azam inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ikiwa na alama 27 huku vinara wa ligi Simba SC, wakiwa na alama 29. Mabingwa watetezi Yanga SC watakuwa dimbani pia kucheza na Ruvu Shooting.

No comments:

Post a Comment