Monday 4 December 2017

Mbunge amchumbia mwanaume mwenzie Bungeni



Tim Wilson

Mbunge mwanamume nchini Australia ameposa kwa mpenzi wake wa kiume wakati wa kikao cha bunge cha kujadili kuhalalishwa ndoa za jinsia moja.

Tim Wilson alimchumbia Ryan Bolger ambaye alikuwa ameketi eneo la umma. Wawili hao wamekuwa wapenzi kwa miaka 9.

Mswada huo wa kuhalalisha ndoa ya jinsia moja uliwasilishwa bungeni siku ya Jumatatu baada ya kupitia bunge la Senate wiki iliyopita.

"Katika hotuba yangu ya kwanza, ninatambua uhusiano wetu kwa pete iliyo kwenye mikono yetu yote ya kushoto. Pete hii ni jibu kwa maswalii ambayo hatutawezi kuyauliza," Bw Wilson alisema.

"Kwa hivyo kuna kitu kimoja tu ambacho kimebaki kufanywa. Ryan Patrick Bolger utakubalia nikuoe ?"

Swali hilo lilizua shangwe na pongezi, kaala ya Bw Bolger kujibu kwa sauti na kusema "ndiyo"
Mapema Bw. Wilsni alizungumzia maisha yake ya kukua kama kijana mpenzi wa jinsia moja na kukumbana na unyanyapaa .

Bw Wilson ni miongoni mwa wabunge 77 ambao watajadili mswada huo.

No comments:

Post a Comment