Tuesday 5 December 2017

VIDEO: Polisi wamnasa komandoo wa Burundi akiwa na AK.47 akifanya matukio ya ujambazi


Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es alaam mnamo tarehe 28/11/2017 na tarehe 30/11/2017 askari walifanya oparesheni maalum ambayo ilifanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa watatu ambao wanajihusisha na matukio ya uporaji na mauaji mbalimbali katika jiji la Dar es salaam.

TAZAMA FULL VIDEO HAPO CHINI.....USISAHAU KUSUBSCRIBE

Kamanda SACP Lazaro Mambosasa amesema hayo leo  alipozungumza na waandishi wa habari, na kusema kuwa baada ya  mahojiano name watuhumiwa hao walikubali kuonyesha silaha moja aina ya AK.47, Magazine mbili 2 na risasi 57 ambayo walikuwa wameificha kwenye kichaka karibu na eneo la Ubungo Mawasiliano, pia walionyesha pikipiki mbili aina ya Boxer zenye namba za usajili MC 757 BCT rangi nyekundu na MC 946 BSE  rangi nyeusi ambazo walizipora katika matukio mbalimbali.


Pia Kamanda Mambosasaaliongeza kuwa walipohojiwa zaidi walisema wanazo silaha nyingine ambazo wamezificha kwenye kichaka eneo la Ununio na wako tayari kwenda kuonyesha silaha hizo, walipofika huko wakati wakishuka kwenye gari jambazi mmoja raia wa Burundi aliyefahamika kwa jina la Fanuel Luchunda Kamana @Mrundi alimvamia askari kwa lengo la kumpora silaha huku wenzake wawili wakijaribu kutoroka na ndipo walijeruhiwa kwa risasi.

Aidha majambazi hao waliwahishwa katika hospitali ya Mwananyamala ili kupatiwa matibabu na ndipo madaktari wakabaini kuwa tayari wameishafariki dunia.

Miili hiyo imehifadhiwa hospitalini hapo kwa hatua za uchunguzi wa kitaalamu, aidha majambazi hao walikiri kufanya matukio kadhaa ya uporaji na mauaji likiwemo tukio la mauaji huko Kunduchi Mtongani la tarehe 19/11/2017 ambapo huwaua madereva bodaboda na kupora pikipiki zao na kuziuza kwa TSHS.800, 000/=.

Majambazi wengine waliofariki ni Gallus Clement, (31) na Fredrick Wilbord Acholo mkazi wa Gongo la Mboto.

No comments:

Post a Comment