Wednesday 6 December 2017

Moto mkubwa wazuka California



Karibu watu 27,000 walilazimishwa kukimbia manyumba yao usiku wa manane wakati moto mkubwa ulisamba kwa haraka kusini kwa jimbo la Carlifonia.

Watu wamehamishwa kwa lazima kutoka makwao katika miji ya Ventura na Santa Paula karibu kilomita 115 Kaskazini mwa Los Angeles.

Wazima moto walionya kuwa moto huo ulikuwa unasambaa kwa haraka na hawangeweza kuuzima.

Ukichochewa na upepo mkali moto uliosambaa ukubwa wa maelfu ya ekari kwa saa chache.

Gavana wa California Jerry Brown ametangaza hali ya tahadhari katika kaunti ya Ventura akiihaidi kukukabili moto huo kwa vyoyote vile.

Mapema iliripotiwa kuwa mtu mmoja alifariki kwenye ajali ya barabarani akijaribu kuukimbia moto huo, lakini idara ya wazima moto kaunti ya Ventura imesema kuwa hakuna mtu aliyepatikana kwenye gari hilo lilikuwa limepinduka.

Maafisa walisema kuwa mzima moto alijeruhiwa. Pia walisema kwa nyumba 150 zilikuwa zimeharibiwa na watu 260,000 walikuwa hawana umeme.

No comments:

Post a Comment