Tuesday 5 December 2017

Tanga: Kifaa cha kujifunzia Kingereza chasambazwa


Wadau mbalimbali wa elimu kwa kushirikiana na Serikali wamesambaza vifaa maalum vya kufundishia somo la Kingereza mashuleni ili kusaidia kumaliza changamoto na kuongeza uelewa kwa wanafunzi wa sekondari mkoani tanga.

Kifaa hicho kijulikanacho kwa jina la E.rider kitaanza kutumika rasmi kwa mwaka 2018,huku mtaalamu kutoka shirika la CAMFED ambao ndio wametoa vifaa hivyo anasema kifaa hicho kina uwezo wa kuhifadhi jumla ya vitabu elfu moja na mia nne kwa wakati mmoja.

Kwa upande wa  Mwakilishi wa Afisa Elimu mkoa wa Tanga ametoa wito kwa walimu waliokuwa wakipewa mafunzo ya kutumia kifaa hicho huku kamera ya ITV ikushuhudia mwitiko huo wa waakimu.

 Wadau hao wamefanya  kitendo hicho baada ya kuonekana kuwa lugha ya kingereza imekuwa ni kikwazo kwa wanafunzi wanaofaulu shule za msingi kwenda sekondari hasa mkoani Tanga.

No comments:

Post a Comment