Wednesday 6 December 2017

Facebook yazindua mtandao wa kijamii wa watoto



Kampuni ya Facebook imezindua mtandao mpya wa kijamii wa kutumiwa na watoto wa chini ya miaka 13.

Mtandao huo ambao umeundwa kwa njia sawa na mtandao wa Messenger ambao huwawezesha wanaoutumia kuwasiliana kwa kutumiana ujumbe utakuwa ukiitwa Messenger Kids.

Facebook kwa kawaida imekuwa hairuhusu watoto wa chini ya miaka 13 kutumia mtandao wake mkuu wa Facebook.

Lakini taarifa zinasema wapo wengi ambao huhadaa kuhusu umri wao na kwamba inakadiriwa watoto zaidi ya 20 milioni wa chini ya miaka 13 wanatumia mtandao wa Facebook.

Messenger Kids inatarajiwa kuwapa watoto ufahamu kuhusu nembo ya Facebook na hivyo kuongeza uwezekano wao kusalia kwenye mtandao huo. Facebook wamechukua hatua hiyo huku wakiendelea kupata ushindani mkali kutoka kwa Snapchat.

Facebook wamesema utafiti unaonesha wazazi wako radhi kuwaruhusu watoto wao wa miaka 6 hadi 12 watumie mitandao ya kijamii, mradi wawe wanaweza kufuatilia watoto wao wanafanya nini.

Facebook imeongeza uwezo wa kuhariri picha na video kuzifanya ziwavutie watotoHaki miliki ya
Facebook imeongeza uwezo wa kuhariri picha na video kuzifanya ziwavutie watoto
Facebook Messenger Kids itahitaji wazazi kuwafungulia watoto wao akaunti na pia ndio watakaoidhinisha ni watoto gani wanaweza kuwa marafiki wa watoto wao.

Akaunti ya mtoto inaweza kusimamia na mzazi kwa kutumia akaunti yake ya Facebook.

Watoto wataruhusiwa kuwasiliana kwa video, kutuma picha, video na arafa kwa marafiki zao ambao wameidhinishwa na wazazi wao.

Kwa sasa, mtandao huo wa kijamii utapatikana Marekani pekee na kwa watu wanaotumia iOS au simu na mitambo ya Apple.

No comments:

Post a Comment