Thursday 7 December 2017

Pam D afunguka kuhusu Ney Wamitego


MWANADADA ambaye anafanya vizuri kwenye gemu la Muziki wa Bongo Fleva, Pamela Daffa ‘Pam D’, amefunguka juu ya skendo ya kujichimbia na mwanamuziki Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ hotelini wakiwa kwenye ziara ya kimuziki katika mikoa mbalimbali hivi karibuni na kudai hazina ukweli.


Akichonga na Showbiz-Xtra kuhusiana na ishu hiyo, Pam D alisema mara nyingi wakiwa na Nay, kila mmoja anakuwa analala kwenye chumba chake na kilichokuwa kimewapeleka kwenye mikoa hiyo ni kazi na wala si kitu kingine.

“Hayo maneno si ya kweli kabisa bhana, mimi nilikuwa ninalala kwenye chumba changu na Nay kwenye chumba chake kwa hiyo hakuna ukweli wowote ule, sisi ni washkaji tu sijui kwa nini watu wamejiaminisha kwamba sisi ni wapenzi,” alisema Pam D.

No comments:

Post a Comment