Friday 8 December 2017

Akamatwa na Polisi baada ya kumuua nesi



Polisi siku ya Jumatano walimkamata mgonjwa aliyemuua nesi kwa kumpiga risasi ya kichwa kwenye kituo cha afya cha Chiromo huko Westlands, Nairobi

Mgonjwa huyo aliyetambuliwa kwa jina la Joseph Njoroge Mungai mwenye kibali cha kumiliki silaha alimpiga risasi ya kichwa daktari huyo aliyefahamika kwa jina la Faustine Mwandime Mwandilu

Kamanda wa polisi wa Nairobi Japheth Koome amesema mtuhumiwa atapelekwa mahakamani kwa kesi ya mauaji

Mtuhumiwa huyo mwenye matatizo ya akili alipelekwa na kulazwa hospitalini hapo akiwa na bunduki baada ya kukataa kuiwasilisha kwa walinzi wa hospitali

No comments:

Post a Comment