Tuesday 5 December 2017

California yakumbwa na moto mkali


Mtu mmoja ameripotiwa kupoteza maisha huku maelfu ya watu wakiwa wamekimbia manyumba yao kutokana na moto mkali ulioikumba California

Kwa mujibu wa habari,moto huo umesababishwa na hali ya hewa iliyosababisha moto ho kusambaa kwa kasi.

Moto huo wa "Thomas" unasemekana kuchochewa na upepo mkali,hali ambayo inausababisha kusambaa kuelekea mji wa Ventura.

Ripoti zinaonyesha kuwa moto huo unasambaa kwa kasi na manyumba pamoja na mali za watu vipo katika hatari ya kuangamizwa.

Mpaka sasa watu 27,000 tayari wameyahama makazi yao.

Moto huo umeripotiwa kuwa ni hatari na umekuwa vigumu kuudhibiti.

No comments:

Post a Comment