Saturday 20 January 2018

VIDEO: Mtulia Uso Kwa Uso Na Meneja

Aliyekuwa meneja wa kampeni wa Maulid Mtulia kwenye uchaguzi wa 2015 Kinondoni,  Rajabu Salim Jumaa amerejesha fomu ya kuombea kuteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwania nafasi hiyo.

Jumaa ambaye amerejesha fomu hizo leo Januari 20, 2018 katika ofisi ya uchaguzi  wa jimbo la Kinondoni iliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam, amesema hatua ya Chadema kusimamisha mgombea katika uchaguzi huo ni kudhoofisha upinzani.

Mwaka 2015 mgombea wa CUF Mtulia alishinda ubunge wa jimbo hilo lakini alijivua uanachama wa CUF na kuhamia CCM na hivyo kupoteza sifa ya ubunge. Hata hivyo Mtulia amepitishwa na chama hicho tawala kugombea ubunge katika jimbo hilo, leo anatarajia kurejesha fomu za NEC.

Jumaa ambaye yupo CUF upande unaomuunga mkono mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, amesema hatua ya Chadema kusimamisha mgombea katika uchaguzi huo ni kudhoofisha upinzani.

"Chadema wanakuja kupoteza nguvu na kuja kugawa kura za wapinzani. CUF ililipata jimbo la Kinondoni kukiwa na ushirikiano wa Ukawa na siyo mtu mmoja.

Chama kilichoshirikiana katika mchakato huo bado kipo na kimemsimamisha mgombea iweje leo Chadema wamesimamisha mgombea," amehoji.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......... USISAHAU KUSUBSCRIBE

No comments:

Post a Comment