Thursday 18 January 2018

Mkali wa tennis Uingereza atupwa nje ya michuano



Mchezaji tennis namba moja kwa viwango vya ubora nchini Uingereza mwanadada, Johanna Konta ameondolewa kwenyemichuano ya Australia Open baada ya kufungwa na mchezaji anaeshikilia nafasi 123 duniani, Bernarda Pera.

Mmarekani, Bernarda Pera amemshinda Konta kwa jumla ya seti 6-4 7-5 katika kipindi cha pili cha mchezo.

Mara baada ya kutolewa katika mashindano hayo Konta amesema “Ni jambo la kusisimua lakini tunaendelea vizuri na benchi langu la ufundi, siji sikii vizuri lakini kwa namna yoyote lazima nikubali matokeo,”Konta.

Konta ameongeza “Nimecheza kila namna mpaka kufikia pale kwa hakika sikuhitaji rejea nyumbani mapema.”

No comments:

Post a Comment