Saturday 20 January 2018

Diwani afariki dunia Kwimba



Diwani wa Kata ya Lyoma katika Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza, Julius Samamba (CUF), amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Taarifa kwa umma iliyotelewa leo Ijumaa (jana) na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Pendo Malebeja imeeleza kuwa diwani huyo alifariki dunia Januari 16 akiwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza alikolazwa kwa matibabu.

“Mazishi ya marehemu yanatarajiwa kufanyika leo Januari 19 katika kijiji cha Kimiza kata ya Lyoma,” anasema taarifa hiyo.

Pamoja na kutoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki, madiwani na watumishi wa halmashauri hiyo, Malebeja amesema kifo cha diwani huyo kuwa pigo kwa halmashauri kutokana na umahiri na uwezo aliokuwa nao katika kujenga na kusimamia hoja kwenye mijadala ya masuala ya maendeleo.

Source: Mwananchi

No comments:

Post a Comment