Saturday 20 January 2018

Mapenzi yamtesa Kajala kisa mwanaye



STAA wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja amefunguka kuwa hivi sasa anaumizwa na mapenzi ya kufichaficha kwa sababu ya kulinda heshima yake kwa mtoto wake wa kike, Paula kwa kuwa sasa amekuwa msichana mkubwa.

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Kajala alisema amekuwa kwenye wakati mgumu sana wa kuwa na uhusiano wa kificho lengo likiwa ni kutomharibu mwanaye huyo ambaye ana uelewa mkubwa na anatambua kila kitu.

“Sipendi Paula anijue kiundani kuhusiana na mahusiano kwa sababu kwa umri aliofikia na darasa alilopo (Kidato cha nne) kama sitakuwa na usiri ataelewa kila kitu, sio Kajala yule tena wa zamani wa kuweka mpenzi wazi ingawa inaniumiza kwani sikuzoea, na mapenzi ya siri yanaumiza asikwambie mtu,” alisema Kajala.



No comments:

Post a Comment