Saturday 20 January 2018

DALILI ZA MIMBA KUTUNGA NJE YA MJI WA UZAZI


HILI ni tatizo ambalo linawaathiri wanawake wengi. Kwa kawaida, mimba zinazotungwa nje ya mfuko wa uzazi hazina uwezo wa kukua kuwa mtoto kamili. Mimba hizi ni hatari kwa afya ya mjamzito kwa vile humfanya kupoteza damu nyingi na hatimaye kusababisha kifo asipowahi kutibiwa. Katika mfumo wa uzazi wa mwanamke, kuna sehemu nyingi ambazo kila moja ina umuhimu wake.

Ikiwa sehemu mojawapo itapata hitilafu, husababisha athari katika mfumo wa uzazi. Miongoni mwa sehemu muhimu ni ovari ambayo ndiyo sehemu mayai ya uzazi yanapotengenezwa. Mayai haya husafiri kupitia mirija ya fallopian.

Kazi za mirija ya fallopian ni kusafirisha mayai kutoka katika kiwanda chake cha uzalishaji (ovari) mpaka kwenye mfuko wa uzazi (uterus). Utungisho wa yai la kike (ovum) na mbegu ya kiume (sperm) hufanyika kwenye mirija hii.

Mara baada ya utungisho, misuli inayozunguka mirija ya fallopian ikishirikiana na vinyweleo vilivyopo ndani ya mirija hii husukuma kiinitete au yai lililorutubishwa na kulipeleka kwenye uterus. Yai lililorutubishwa au
kiinitete, lifikapo kwenye uterus hujipachika katika mojawapo ya kuta zake kwa ajili ya kuendelea kurutubishwa, kukua taratibu na hatimaye kufanya mtoto.

No comments:

Post a Comment