Thursday 18 January 2018

Batuli awataka mastaa kumrudia Mungu


Yobnesh Yusuph ‘Batuli’.

MSANII mwenye mvuto Bongo Muvi, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ amewasihi wasanii wenzake wajaribu kumrudia Mungu japo mara moja kwa wiki.

Akizungumza na Showbiz Xtra, Batuli alisema kuwa anatambua mastaa wengi wamesahau kusali kabisa na kujua kama kuna Mungu huku wakiendelea kufanya vingi vya kidunia.

“Jamani hakuna kitu kizuri kama kuona staa akiwa kanisani au msikitini yaani hata jamii inakuchukulia kwa mtazamo wa tofauti kabisa, tumrudie Mungu,” alisema Batuli.


No comments:

Post a Comment