Friday 19 January 2018

Madiwani waliohama Upinzani kugombea tena kupitia CCM Ruangwa


Madiwani wa Kata za Namichiga na Nachingwea Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi Bakari Omari Mpanyangula na Mikdadi Ibadi Mbute, ambao walihama vyama vya Chadema na CUF na kujiunga na Chama cha Mapindizi CCM kwa kukiunga mkono Chama hicho.

Madiwani hao wananafasi kubwa ya kugombea tena nafasi hiyo kupitia CCM kwani umedhihirishwa Leo na Katibu wa CCM mkoa wa Lindi Bw, Loti Olelesele kwenye hafla ya kuwakabidhi kadi za chama hicho iliyofanyika kwa nyakati tofauti katika kata za Nachinwea na Namichiga.

Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya Wanachama na wapenzi wa CCM katika kata hizo Olelesele alisema Mpanyangula na Mbute ndio wanachama wanaofaa kugombea nafasi hiyo tena kupitia chama hicho, kwakuwa wameonesha uwezo mkubwa wa Uongozi walipokuwa Madiwani kupitia Vyama walivyohama.

Pia Olelesele alisema licha ya kuonesha uwezo wa uongozi lakini pia wanakubalika na Wananchi hali ambayo ilisababisha wawabwage wagombea wa CCM katika uchaguzi Mkuu uliopita "Tunakubaliana na uamuzi wa Vikao halali vya Chama vya kata za Namichiga na Nachingwea vilivyopendekeza wawe wagombea wetu wakati wa uchaguzi mdogo kwenye kata hizo kwani wananchi wameendelea kuwaamini," alisema Olelesele.

Lakini pia alitumia hafla hiyo kuwahakikishia Wananchi kwamba Chama hicho kimeweza kudhibiti vitendo vya rushwa  hivyo Viongozi wanapatikana kutokana na uwezo wao na kukubalika kwao mbele ya Wananchi


Nae Katibu wa Mkoa wa Lindi wa Jumuia ya Wazazi wa Chama hicho Tatu Hamisi, ameipongeza Serikali kwa kutekeleza ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa vitendo ikiwamo sera ya Elimu bila malipo, alitoa wito kwa wazazi kutumia vyema fursa hiyokwa kuwapeleka watoto wao Shule.

Hata hivyo Wanachama 15 kutoka upinzani walihama vyama vyao na kujiunga na CCM na kukaribishwa na makada wa chama hicho, nae Mpanyangula akifuatwa na watu sita wa Familia yake walimuunga mkono, Mpanyangula alisema"pamoja na kuridhishwa na Serikali ya awamu ya tano lakini mgogoro wa Uongozi ndani ya CUF umesababisha chama hicho kukosa muelekeokuanzia juu mpaka chini hivyo huu ni mwanzo tu wanachama wengi wanajiandaa kuhama," alisema Mpanyangula.

Madiwani hao walitangaza kuvihama vyama vyao vya awali wiki iliyopita kwa madai kwamba wamehamia CCM ili kuungana na Serikali ya awamu ya tano na Mbunge wao Mheshimiwa Kassim Majaliwa katika kuwaletea Wananchi maendeleo.





No comments:

Post a Comment