Saturday 20 January 2018

Mawaziri Wakutana Dar Kuanza Kutekeleza Ujenzi wa Reli

Mawaziri wa Miundombinu na Uchukuzi kutoka Tanzania na Rwanda wamekutana leo jijini Dar es salaam kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa maelekezo ya Marais wa nchi hizo mbili yaliyotolewa hivi karibuni kuhusu na makubaliano ya Ujenzi wa Reli ya kisasa ya yenye urefu wa kilomita 572 itakayoanzia Isaka mpaka Kigali Rwanda.Katika mazungumzo yao, mawaziri hao wameridhia kwa pamoja rasimu ya kujenga reli ya kisasa kwa lengo la kuendeleza uhusiano wa nchi hizo mbili, ikiwa ni pamoja na kurahisisha na kupunguza gharama za usafirishaji, kuunganisha miundombinu, kukuza za uchumi na kutoa huduma bora kwa wakazi ws ukanda huu.

Kata hatua nyingine, Mawaziri Dk Augustine Mahiga na Waziri wa Fedha Philip Mpango ambao ni miongoni wa Viongozi waliohudhuria mazungumzo hayo wamesema ujenzi wa Reli hiyo ya kisasa baina ya Tanznaia na Rwanda itakuwa ni kiungo muhimu cha kuleta maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wa nchi hizo.

No comments:

Post a Comment