Tuesday 5 December 2017

Kampuni ya CNBM Group yaunga mkono jitihada za Makonda



Kampuni ya China Nationali building Material Group leo imekabidhi hundi ya Shilingi Milioni kumi ili kuunga Mkono juhudi zinazofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kusaidia Watu wenye uhitaji wa miguu bandia na zoezi la upimaji afya.


Akizungumza na Waandishi wa habari leo mara baada ya kupokea msaada huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa,  Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Dakta Grace Magembe amesema Serikali ya Mkoa imekusudia kutatua changamoto za kiafya kwa wananchi pamoja na kusaida watu wenye ulemavu,ambapo amebainisha kuwa hapo awali Serikali ya Mkoa ilikusudia kusaidia watu wenye ulemavu miambili lakini idadi ya wenye uhitaji wa miguu ni zaidi ya watu elfu moja hivyo amewataka wadau kuendelea kujitokeza kusaidia.

Dakta Magembe ameongeza kuwa tokea kuingia madarakani Serikali ya awamu ya tano iliyo chini ya Rais Dakta John Magufuli imekuwa ikishughulikia changamoto mbalimbali za wananchi hivyo amewataka wananchi kuendelea kuunga mkono jitihada za serikali

Kwa upande wake Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya China National building Material Group Wang Shupeng amesema kampuni hiyo imeridhishwa na juhudi zinazofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam na imetambua umuhimu wa kusaidia watu wenye mahitaji maalumu ikiwemo miguu bandia hivyo mbali na msaada huo wa shilingi milioni kumi za kitanzania itaendelea kutoa misaada mbalimbali kuunga mkono serikali.

No comments:

Post a Comment