
Kiungo mshambuliaji wa Ndanda FC, Mrisho Ngassa, amesema kuwa amechoka usumbufu wa kuidai klabu yake ya zamani, Mbeya City, mshahara wake wa miezi minne, lakini akasisitiza anaomba fedha zake.
Ngassa alijiunga na Ndanda hivi karibuni katika usajili wa dirisha dogo akitokea Mbeya mara baada ya mkataba wake kumalizika kabla ya kugoma kumuongezea mwingine.
Ngassa alisema kuwa anaidai klabu hiyo shilingi milioni 4.8 alizotakiwa alipwe tangu Desemba, mwaka jana.
Ngassa alisema amefikia hatua ya kuweka wazi madai hayo baada ya hivi karibuni viongozi wa timu hiyo kumwambia watampatia fedha hizo baada ya kulipwa fedha kutoka Azam TV ambao wanadhamini klabu za ligi kuu.
“Nimechoka kuongopewa na viongozi wa Mbeya City, kwani kila wakati nikiwapigia simu kudai malipo yangu ya mshahara ambayo ni shilingi milioni 4.8 wamekuwa hawapokei simu.
“Lakini hata wakipokea wakati mwingine wananipiga Kiswahili, kwa maana ya kunitajia siku nyingine na hivi karibuni walinipa maneno mazuri ya kuwa watanilipa fedha zangu baada ya wao kulipwa na Azam TV.
“Ninajua tayari wamepatiwa fedha hizo, lakini wamejikausha kunilipa fedha hizo ambazo ninadai hadi leo (jana Jumapili), hivyo nimechoshwa nao, naomba wanilipe fedha zangu,” alisema Ngassa aliyewahi kuzichezea Simba, Yanga na Azam FC.
Alipotafutwa jana mchana, Katibu Mkuu wa Mbeya City, Emmanuel Kimbe, alisema hayupo katika nafasi nzuri kuzungumzia suala hilo.








Kikosi cha Yanga kitakachovaana na Azam FC leo
Rais Joseph Kabila amepinga ukosoaji unaotekelezwa na jamii ya kimataifa kuhusu kucheleweshwa kwa uchaguzi katika jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Kampuni moja ya rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe inatakiwa kuondoka katika kipade kimoja cha ardhi kinachomilikiwa na shule moja la sivyo ishtakiwe.
Timu ya Mbeya City
Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Edward Lowassa jioni leo amemnadi Mgombea wa Ubunge wa Kinondoni kupitia chama hicho, Salumu Mwalimu huku akiwataka wakazi wa Kinondoni kuacha kumuongelea mgombea wa CCM, Maulid Mtulia maana amekuwa msaliti kwao.
Mlipuaji wa kujitolea mhanga amewaua takriban watu 95 na kuwajeruhi wengine 158 katika mji mkuu wa wa Afghanistan Kabul, kulingana na maafisa.
Shirika la kimataifa la msalaba mwekundi limesema kuwa utumizi wa 'ambulence' unakera.Wiki moja iliopita ,wapiganaji wa Taliban waliwaua watu 22 katika hoteli moja ya kifarahari mjini Kabul.