
''Kumtoa Ronaldo lilikuwa ni suala la kiufundi wala si kumpumzisha kwaajili ya mchezo dhidi ya PSG kama inavyodaiwa, tulikuwa tunaongoza kwa 2-1 na hatukuweza kuongeza bao licha ya kushambulia, hivyo tulitaka kuingiza kiungo Marco Asensio ili tumiliki mpira'', amesema.
Zidane amelazimika kutoa ufafanuzi huo baada ya kuwepo kwa malalamiko mengi kutoka kwa mashabiki ambao wanadai kutoka kwa Ronaldo kulisababisha Levante kushambulia na kusawazisha bao la pili dakika ya 89 na kufanya mchezo umalizike kwa sare ya 2-2.
Baada ya sare ya jana Real Madrid imesalia katika nafasi ya nne ikiwa na alama 39 huku vinara Barcelona wakiwa na alama 57 kileleni.
No comments:
Post a Comment