Monday 22 January 2018

Kagera Sugar imejiandaa kuikwamisha Simba


Klabu ya Simba SC leo inarejea kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, sehemu ambayo ina kumbukumbu ya kukwamishwa mipango yake ya kusaka ubingwa msimu uliopita.

Kocha wa Kagera Sugar Meck Mexime, amesema timu yake imejiandaa kwa muda mrefu hivyo leo inaingia uwanjani kupambana na vinara wa ligi Simba SC huku lengo likiwa ni kusaka alama tatu.

''Hali ya hewa leo hapa Bukoba ni jua tu na hali ya uwanja ni nzuri, tumefanya maandalizi kwa muda mrefu leo tuna kazi moja tu ya kucheza mpira kwaajili ya kupata alama tatu kwasababu mpira ndio kazi yetu'', amesema Mexime.

Timu hizo zinakutana kwenye mchezo wa raundi ya 14 ambapo Simba wanahitaji alama tatu ili kuweza kurejea kileleni mwa msimamo wa ligi. Simba kwa sasa ina alama 29 nyuma ya Azam FC yenye alama 30.

Msimu uliopita Simba ikiwa inaelekea kwenye hatua za mwiosho za kusaka ubingwa ilitibuliwa mipango na Kagera Sugar April 2, 2017 ilipokubali  kipigo cha mabao 2-1 hivyo kuiacha Yanga katika mazingira mazuri ambayo mwisho wa ligi waliibuka mabingwa.

No comments:

Post a Comment