Monday 22 January 2018

Baada ya kuona picha ya mtoto akiomba jezi yake, Samatta afunguka


 Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars anayecheza soka la kulipwa katika club ya KRC Genk ya Ubelgiji Mbwana Samatta licha ya kuwa nje ya uwanja kwa miezi miwili lakini ameonesha kuzidi kupendwa na mashabiki wa club yake.

Moja kati ya ujumbe unaosambaa kwa sasa katika mitandao ya kijamii ni pamoja na post ya bango ya shabiki mtoto wa KRC Genk ikiwa imeandikwa “Mbwana Can I have Your Shirt Pendeza” akiwa kamaanisha “Mbwana unaweza kunipa jezi yako? Pendeza”

Baada ya Mbwana Samatta kuona post ya picha ya mtoto huyo akajibu “Ndio naweza kukupa kwa nini ishindikane” hiyo imezidi kudhihirisha mapenzi ya dhati ya mashabiki kwa Mbwana Samatta maana sio kila mchezaji soka huwa anapata nafasi ya kupendwa na mashabiki kwa kiwango hicho.

No comments:

Post a Comment