Monday 22 January 2018

AT: Tuzo zangu za Marekani siwezi kuzipasua


Msanii wa muziki Bongo, AT amesema hawezi kuzipasua tuzo zake alizoshinda nchini Marekani November mwaka jana, 2017.

Muimbaji huyo katika mahojiano na kipindi cha Leo Tena cha Clouds Fm amesema awali alipanga kupasua tuzo zake za Kilimanjaro Music Award (KTMA) zilizokuwa zikitolewa hapa nchini lakini baadaye akagundua kuwa tuzo hizo ni mali ya Baraza la Sanaa Taifa (BASATA).

“Ni baada ya kuomba msaada ili nisaidiwe kwenda Kongo nikafanye kolabo na Koffi Olomide, wakanizungusha sana, ilikuwa hasira tu, ila hizi tuzo zangu za Marekani siwezi kuzipasua,” amesema AT.

November mwaka jana AT alishinda tuzo mbili katika ‘B&K Music & Video Music Awards’, vipengele alivyoshinda ni International Artist na Best Music Video kupitia wimbo wake ‘Sili Feel’.

No comments:

Post a Comment