Friday, 1 December 2017

Jay-Z akiri kuchepuka kwenye ndoa yake



Jay-Z na mke wake Beyonce

Mwanamuziki wa rap Jay -Z amekiri kwamba alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanawake wengine akiwa bado kwenye ndoa yake na Beyonce.

Amekiri hilo kwa mara ya kwanza alipokuwa akihojiwa kuhusiana na maisha yao na jarida moja.

Aliambia jarida la Style la gazeti la The New York Times kwamba alijiwekea vizuizi kutokana na matatizo aliyokumbana nayo alipokuwa mtoto, jambo ambalo lilimfanya kujifungia na kuwa uzinifu.

''Kitu kigumu ni kuona uso wa mtu uliojaa huzuni uliosababishwa na wewe, alisema Jay -Z."

Wanandoa hao walikuwa wamedokeza kuhusu Jay-Z kutokuwa mwaaminifu kwenye nyimbo zao.

Mwanamuziki huyo amesema kwamba wangetalikiana lakini alipata ushauri nasaha ili kumsaidia kukabiliana na matatizo yake ya hapo awali.

Kama unavyofahamu, watu wengi hutalikiana, na visa vya kutalikiana ni takriban asilimia 50 mambo kama haya yanapotokea.

Mwaka wa 2013, kulikuwa na uvumi kwamba mwanamuziki huyo wa nyimbo za rap hakuwa mwaminifu kwa mke wake na ilichochewa na kitambulisha mada cha #elevatorgate pale Solange Knowles alipomshambulia Jay -Z, huku Beyonce akionekana kunyamaza kimya.

Albamu ya hivi majuzi ya Jay -Z ya 4:44 ilizungumzia yeye mwaminifu.

Aliandika :''Naomba radhi / kwa kutoka nje ya ndoa/aliyemfanya mtoto wangu kuzaliwa kupitia kwa macho ya mamake.''

Mwaka mmoja kabla ya albamu hiyo ya 4:44 kuzinduliwa , Beyonce aliimba kuhusu ''Becky with good hair (Becky mwenye nywele nzuri)'' kwenye albamu yake ya Lemonade.

''Yeye hunihitaji wakati sipatikani, heri ampigie Becky ambaye ana nywele ndefu.''

Jay -Z na Beyonce walikuwa wamepanga kutoa albamu ya pamoja badala yake wakaishia kufanya nyimbo kila mmoja yake.

''Tunatumia sanaa kujiliwaza. Tulianza kutunga nyimbo zetu pamoja. Na nyimbo alizokuwa akibuni wakati huo zilikuwa mbele sana.

''Kwa hivyo albamu yake ilizinduliwa kinyume na matarajio ya kuwa albamu hiyo ingekuwa imewashirikisha wanandoa hao.

Pia Jay-Z hakuzungumzia kuhusiana na ndoa yake pekee, pia alizungumzia kuhusiana na mahusiano yake na Kanye West.

''Nilizungumza na Kanye wakati mmoja, kumwambia yeye ni kama kakangu. Nampenda Kanye. Kwa kweli. Ni mahusiano tata kati yetu.

Alikubali kwamba hawajakuwa na uhusiano rahisi.

Kanye West aliripotiwa kuacha kazi katika kituo cha umiliki wa huduma ya kusikiliza muziki ya moja kwa moja ya mwanamuziki ya Jay Z, Tidal ,kuhusiana na mzozo wa kifedha.

''Niko na uhakika anahisi nimemfanyia mambo kadhaa pia yeye.

''Natumai tutakapofika umri wa miaka 89, tutaangazia haya baada ya miezi sita au wakati wowote na kutafurahia haya yote.''

Kampuni ya Ford kuachana na magari ya zamani

BOSI mpya wa kampuni ya magari aina ya Ford ya Marekani, ametangaza kuingia katika mpango wa kushindana katika soko kwa kuachana na aina ya magari iliyozoea kuzalisha ‘miaka nenda rudi.’

Bosi huyo, Jim Hackett, katika mikakati yake anasema analenga katika magari ya mfumo mpya unaoegemea zaidi matumizi ya umeme.

Hackett anasema, pia kampuni hiyo kupitia uzalishaji huo na mikakati mingi inatarajiwa kupunguza gharama za uzalishaji kwa wastani wa Dola za Marekani bilioni 14.    Mtendaji huyo mkuu anasema ni maamuzi yaliyofikiwa, baada ya kufanyika tathmini ya siku 100 kuhusu uzalishaji na hali ya soko.

Hackett aliingia ofisini mwezi Mei mwaka huu, akichukua nafasi ya mtangulizi wake Mark Fields, aliyedumu katika nafasi hiyo kwa miaka mitatu.

Inaelezwa kwamba, katika zama za Mark licha ya kampuni kupata faida kubwa, lakini nafasi yake katika soko la magari kimataifa ilianguka sana.

Wataalamu wa masoko kimataifa wanasema nafasi ya Ford, ambayo ni kampuni ya Kimarerkani imeshuka katika soko kutokana na ushindani wa kimataifa hasa kutoka  kwa Wachina na mataifa mengine yanayoibuka.

Hackett anasema, wana mpango wa kuhakikisha asilimia 90 ya magari yanayozalishwa yanaingia katika masoko mbalimbali duniani kuchukua nafasi kubwa ya mauzo, hadi ifikapo mwaka 2020.

Pia, katika muundo magari yanayotarajiwa kuingia sokoni itakuwa na vifaa vingi ndani yake kama vile simu, yote ikilenga kumvutia mteja.

Mengine yanayolengwa na kampuni ni maboresho ya kuzalisha magari ya biashara, wagonjwa na mabasi ya abiria Marekani na kwingineko na tayari bosi huyo anasema wameshaingia mkataba na baadhi ya kampuni kuifanya kazi hiyo.

Hackett anasema huko nyuma walisuasua kuingia katika ushindani wa kuweka mfumo wa umeme kwenye magari wakihofia gharama kubwa, lakini sasa Ford imeamua kujitosa katika aina hiyo ya magari ambayo ndio mvuto wa soko uliopo duniani.

Katika kuanzisha hilo, Ford iliingia mkataba na kampuni za kichina kuzalisha magari hayo ya umeme, ikizingatia Wachina walishapiga hatua sokoni na katika uzalishaji.

Haya ndio matukio yaliotikisa mwaka 2017



TANGU mwaka huu uanze kumekuwa na matukio mengi yaliyojitokeza kwa mastaa, ambayo yalileta mshtuko kwenye jamii hususan kwa watu wanaofuatilia masuala ya burudani kwa wasanii, hapa nakuorodheshea matukio hayo.

1.MAKONDA KUWATUMBUA MASTAA ISHU YA DAWA ZA KULEVYA

Ni ishu iliyokuwa gumzo jijini kufutokana na Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda kuwatumbua baadhi ya wasanii kwa kuwataja majina na kuwaita Kituo Kikuu cha Polisi kutokana na kujihusisha na matumizi ya dawa za kulevya. Miongoni mwa wasanii waliokuwepo kwenye orodha hiyo ni Wema Sepetu, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’, Recho kizunguzungu, TID, Petitman, Deogratius Shija, Salma Jabu Nisha, Tunda Sebastian na wengine wengi.

2.WEMA KUHAMA CHAMA

Mwanadada huyu alikuwa mstari wa mbele kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM), hususan kwenye kampeni ya ‘mama ongea na mwanao’ ambayo ilikuwa ikiendeshwa katika kipindi cha uchaguzi, wakimsapoti Makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassan. Lakini ghafla baada ya Wema kupata msala wa kutumia dawa hizo alihama chama hicho na kuhamia Chadema kwa kuhisi CCM ilimtenga baada ya kupata tatizo hilo.

3. NAY KUWEKWA NDANI

Ilikuwa kizaazaa pale mwanamuziki Emanuel Elibarick alipowekwa ndani baada ya kutoa wimbo uitwao Wapo ambao ulionekana kuwakashifu baadhi ya viongozi wa kiserikali. Hata hivyo, ilikuwa ni kauli moja tu ya Rais Dk John Magufuli aliyesema aachiwe na ikawa hivyo. Mwanamuziki huyo alikaa ndani siku moja.

4.ROMA KUTEKWA

Nchi nzima ilizizima kutokana na mwanamuziki wa Hip Hop, Ibrahimu Mussa ‘Roma Mkatoliki’ kutekwa pamoja na mwanamuziki Moni Central Zone na kijana mwingine ambaye alikuwepo studio hapo Tongwe Record, gumzo hilo liliendelea hadi walipopatikana huku kila mmoja akizungumza lake kuhusu nani alifanya utekaji huo.

5. NUH KUACHANA NA NAWAL

Wengi hawakuamini kilichotokea wakawa wanahisi ni kiki baada ya mwanamuziki Nuh Mziwanda kubwagana na mkewe Nawal ambaye amebahatika kupata naye mtoto mmoja Anya. Lakini huo ndiyo ulikuwa ukweli maana baadaye mwanadada huyo alifunga ndoa na mtu mwingine.

6. HARUSI YA JOTI

Taarifa za harusi hiyo zilipoanza kuenea watu walifikiri ni utani. Lakini baadaye Joti na mkewe walipoonekana wakiwa kanisani na picha kutoka vikiwemo vipande vya video huku mitandao ya kijamii ikienea habari zake, kila mmoja aliamini kweli Joti amefunga ndoa na mkewe.

7. BIFU LA HAMISA NA ZARI

Hili ni miongoni mwa matukio yaliyobamba mwaka huu. Bifu hili liliibuka baada ya mwanamitindo Hamisa Mobeto kuweka wazi kwamba alizaa na Mbongo Fleva ambaye ni mzazi mwenza na mjasiriamali Zarinnah Hassan ‘Zari Ze Bossy Lady.” Hata hivyo, baada ya vijembe mitandaoni baadaye suala hili lilionekana la kawaida na kupitwa na wakati.

8. NDOA YA UWOYA NA DOGO JANJA

Taarifa za muigizaji Irene Uwoya kufunga ndoa na Mbongo Fleva, Dogo Janja ziliwashangaza wengi. Ikawa gumzo kubwa ambalo baadaye lilikosa tija baada ya Uwoya kuweka wazi kupitia magazeti ya Global Publishers kwamba hakufunga ndoa bali ni muvi inayotarajiwa kutoka.

9. LULU KUTUPWA JELA

Tukio la muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ kuhukumiwa kwenda jela kwa muda wa miaka miwili kutokana na kesi ya kumuua bila kukusudia muigizaji Steven Kanumba ilikuwa ni gumzo mpya kwenye media (vyombo vya habari). Wengi hawakuamini kama Lulu angeweza kwenda jela, lakini sheria ni msumeno na hivi tunavyozungumza Lulu yupo jela Seregea.

10. DK SHIKA NA ITAPENDEZA

Hadi sasa hili ndilo tukio la funga mwaka. Tukio hili limebamba baada ya kuibuka mzee mmoja aliyevaa nguo za kawaida na sandozi zilizochoka mguuni akitaka kununua nyumba za Saidi Lugumi.

Mzee huyo si mwingine bali Dokta Loius Shika ambaye alijizolea umaarufu kwenye mnada huo na msemo wa ‘mia tisa itapendeza’ na kuweka wazi kwamba ana mabilioni ya pesa kwenye benki tofauti tofauti nje ya nchi, kwa sasa mzee huyo anakula madili ya matangazo likiwemo kutoka Kampuni ya Sokabet.

Mabadiliko ya Simba yasimamisha usajili



WAKATI wanachama wa Klabu ya Simba wakitarajiwa kupewa taarifa kuhusiana na mchakato wa mabadiliko ya uendeshaji wa klabu hiyo ulivyofikia hapo keshokutwa, mkutano huo unadaiwa kusimamisha mchakato wa usajili, imeelezwa.

Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo inayodhaminiwa na Kampuni ya michezo ya kubashiri ya Sportpesa zinasema kuwa, mfanyabiashara maarufu, Mohammed Dewji "Mo" amesitisha kutoa fedha za kusajili wachezaji kutokana na mabadiliko ambayo yanaweza kufanyika tofauti na ilivyopendekezwa hapo awali.

Chanzo chetu kimesema kuwa kwa sasa mazungumzo yote ya kusajili wachezaji yamesimama kwa sababu bilionea huyo amekuwa na wasiwasi huenda mchakato huo hautafanikiwa.

"Kwa mfano suala la Mavugo (Laudit) kutolewa kwa mkopo lilianza kuzungumzwa lakini sasa halieleweki kwa sababu wanaogopa kumuuza na hawajui mbadala wake atapatikana vipi," kilisema chanzo chetu.

Kiliongeza kuwa hata mabadiliko ya asilimia ambazo wawekezaji wataruhusiwa kununua na zile zitakazobakia kwa wanachama zimeonekana kutowafurahisha baadhi ya viongozi na wadau ambao walikuwa tayari kuwekeza fedha zao ndani ya klabu hiyo.

"Simba imekuwa makini sana katika kufanya uamuzi wa masuala mbalimbali hasa ya matumizi ya fedha katika kipindi hiki, wanajipanga kujenga taasisi yenye nidhamu na inayojiendesha kisasa kwa sababu inataka kuonyesha mabadiliko huku pia ikiweka rekodi nzuri uwanjani," alisema kiongozi huyo.

Awali kabla ya kufanyika kwa tathmini, Mo alisema yuko tayari kupewa hisa asilimia 51 kwa thamani ya Sh. bilioni 20 na inadaiwa baadhi ya wafanyabiashara wengine walijitokeza ambao wameahidi kutoa fedha zaidi ya hiyo iliyotajwa na mfanyabiashara huyo wa hapa nchini.

Wakati huo huo wachezaji wa Simba wamepewa likizo ya wiki moja na watarejea tena uwanjani kuendelea kujiandaa kwa ajili ya kushiriki mashindano ya Kombe la Mapinduzi ambayo yatafanyika kuanzia Desemba 30 mwaka huu Zanzibar.

Source: Nipashe

Video | Moni Centrozone – Bongo Super Star.| Mp4 Download

Video | Moni Centrozone – Bongo Super Star.| Mp4 Download


Video | Moni Centrozone – Bongo Super Star.| Mp4 Download





                                                        DOWNLOAD HERE

Audio | Mohombi Ft Fally Ipupa – Zonga Mama.| Mp3 Download

Audio | Mohombi Ft Fally Ipupa – Zonga Mama.| Mp3 Download

Audio | Mohombi Ft Fally Ipupa – Zonga Mama.| Mp3 Download



                                                           DOWNLOAD HERE

Thursday, 30 November 2017

Video | Kassim Mganga – Dalila | Mp4 Downlod

Kassim Mganga - Dalila

Video | Kassim Mganga – Dalila | Mp4 Downlod





                                                                       DOWNLOAD HERE

Audio | Kassim Mganga – Dalila | Mp3 Download

Audio | Kassim Mganga – Dalila | Mp3 Download
Kassim Mganga – Dalila

Audio | Kassim Mganga – Dalila | Mp3 Download


                                         DOWNLOAD HERE

VIDEO: K' Njaro Stars yatamba kutwaa CECAFA


Kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania bara ' Kilimanjaro Stars' kimepaa leo kuelekea Nchini Kenya kushiriki michuano ya Chalengi huku kikitamba kurejea na Kombe . Stars imeondoka na msafara wa watu 30, Wachezaji 23 na Benchi la ufundi likiwa na watu saba.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI.....USISAHAU KUSUBSCRIBE



VIDEO: Picha za watu waliojeruhiwa uchaguzi mdogo - LHRC




Ripoti ya kituo cha sheria na haki za binadamu nchini Tanzania inaonesha ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu umetekelezwa na vyombo vya dola katika uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika nchini katika kata 43.
Ripoti hiyo inasema kuwa viongozi wa vyama vya siasa, wakala wa uchaguzi pamoja na baadhi ya wapiga kura walipigwa na wengine kuwekwa kizuizini wakati wakitekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria katika uchaguzi huo, hatua ambayo imeonesha hali ya wasiwasi katika uchaguzi unaokuja wa serikali za mitaa na uchaguzi Mkuu wa 2020.



Uchaguzi ulifanyika katika kata 43 zilizo kwenye halmashauri 36 za mikoa 19 nchini.

Akizungumza leo Alhamisi Novemba 30,2017 Kaimu Mtendaji Mkuu wa LHRC, Anna Henga amesema uchaguzi ulikuwa na matumizi mabaya ya vyombo vya dola, watu kupigwa, kukamatwa na kujeruhiwa.

"Vitendo hivi vimeripotiwa kufanywa na vyombo vya dola, watu wasiojulikana na watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa vyama vya siasa vikiwemo CCM na Chadema,” amesema.

Amesema kutokana na matukio hayo, vyombo vya dola vinapaswa kufanya uchunguzi wa kina na kuchukua hatua kali za kisheria kwa watakaobainika kuhusika kwa njia moja au nyingine.

Henga amesema matukio hayo yasipokemewa ni kiashiria kibaya na msingi mbaya utakaoathiri chaguzi zingine ukiwemo wa Serikali za Mitaa wa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.


Breaking Newz: Rais Magufuli afanya uteuzi mwingine



 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amteua Bi. Stella Tullo Chagi kuwa Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba wa Wilaya.

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Eng. John Kijazi ametangaza kuwa uteuzi huo Bi. Stella Tullo umeanza rasmi toka Novemba 25, 2017.

Wahamiaji zaidi ya 100 kutoka Ghana waokolewa kutoka Libya



Zaidi ya raia 100 kutoka Ghana walikuwa wanazuiliwa nchini Libya, wamerudi makwao baada ya Serikali kupata ndege ya kuwapeleka nyumbani.

Walienda Libya wakiwa na matumaini ya kufika Ulaya lakini wakasalia kuwekwa katika vituo vya kufungwa kama wahamiaji haramu.

Kurudi kwao kulifuatia hamaki iliyotanda dunia nzima baada ya kanda ya video kuibuka iliyoonyesha Waafrika wakiuzwa kama watumwa nchini Libya.

Viongozi kutoka Afrika na Ulaya wamekuwa wakijadiliana suala hilo katika mkutano nchini Ivory Coast na wameandaa mpango wa pamoja ili kujaribu kutatua shida hiyo

Abdu Kiba: Alikiba amenifanya chambo


Msanii Abdu Kiba ambaye ni mdogo wa Alikiba, amesema kitendo cha yeye kuachia kazi mpya badala ya wasanii wengine wapya waliopo kwenye lebo ya Kings Music iliyo chini ya kaka yake Alikiba ni kama chambo na sio kupendelewa kama wengi wanavyohisi.

Abdu Kiba ameyasema hayo alipokuwa akizungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, na kusema kwamba lebo iliamua kuanza kumtoa yeye ili kuangalia upepo utaendaje, kwani alikaa kimya sana kwenye game licha ya kuwa tayari ana mashabiki wake.
“Nimeanza mimi kutokana na ukimya wa muda mrefu, wasanii wapya wapo lakini isingekuwa vyema kukurupuka kuwaleta, mimi nimetumiwa kama chambo kwamba tuwalete kuangalia na mapokezi yatakuwaje, sio chambo kama nimetupwa”, amesema Abdu Kiba.
Hivi sasa msanii huyo ameachia wimbo wake mpya aliomshirikisha Alikiba unaoitwa 'Single', ambao ni kazi yake yake ya kwanza chini ya lebo ya Kings Music ambayo inamilikiwa na kaka yake Alikiba,