Monday 22 January 2018

Vanessa kuinufaisha familia ya Mbaraka Mwishehe


Msanii wa muziki Vanessa Mdee amebainisha kwa nini familia ya marehemu Mbaraka Mwishehe itanufaika kwa mauzo ya albamu ya Money Monday kwa njia ya mtandao na sio kwa mauzo ya kawaida (CD).

Mrembo huyo amebinbisha hayo kupitia mahojiano aliyofanya na Bongo5 na kusema kuwa ameamua maamuzi hayo yamekuja baada ya kutoa kionjo katika ngoma ya ‘Jogoo la Shamba’ ya marehemu Mbaraka na kukitumia katika ngoma yake ya ‘ Pumzi ya Mwisho’ aliyowashirikisha marapa wawili amabo ni Cassper Nyovest na Joh Makini.

“Familia ya mubaraka itanufaika kwa mauzo ya kimtandao kwa sababu soko letu lina hamia kimtandao Zaidi hivyoi ni meona ni busara kutumia njia hiyo,” amesema Vanessa.

No comments:

Post a Comment