Tuesday 23 January 2018

Chin Bees bifuni na Mganda


Chin Bees.

MSANII wa Bongo Fleva, Chin Bees amejikuta akiingia kwenye bifu zito na msanii wa Muziki wa Uganda, Fik Fameica kwa kumuibia ‘beat’ la wimbo wake wa Pepeta.

Akizungumza na Full Shangwe, Chin Bees amesema kuwa ameshtushwa na kitendo cha msanii huyo kutumia beat lake na kuuita Mafia bila kuzungumza naye.

Fik Fameica

Inaumiza sana kuona msanii anatumia beat lako bila kukushirikisha kwa chochote. Huyo msanii wala simjui na sijaongea naye ila tumewasilisha malalamiko yetu Cosota ili hatua stahiki zichukuliwe.

Full Shangwe ilimtafuta Fik Fameica kwa njia ya WhatsApp na kumsomea mashtaka yake lakini hakujibu chochote zaidi ya kutuma wimbo wake wa Mafia.

No comments:

Post a Comment