Saturday, 27 January 2018

Alichokisema Mr T kuhusu Darassa kuwa teja



Baada ya kimya cha muda mrefu kwa msanii Darassa ambaye mwaka juzi 2016 alitingisha sana na wimbo wake 'Muziki' kumeibuka tetesi kuwa msanii huyo naye amejiingiza katika matumizi ya dawa za kulevya, jambo ambalo limewashtua wengi. 

Kufuatia tetesi hizo mtangazaji wa kipindi cha Bongo fleva Top 20 ya East Africa Radio, Jr Junior alimvutia waya msanii huyo lakini bahati mbaya hakuweza kupokea simu yake jambo ambalo lilimfanya kumpigia simu mtu wake wa karibu ambaye ni producer wake Mr T Touchez ili kufahamu ukweli juu ya tuhuma au tetesi hizo. 

Baada ya Mr T Touchez kupigiwa simu alisema yeye hafahamu lolote juu ya jambo hilo na kukiri kuwa kwa sasa hajakutana na msanii huyo muda kidogo, hivyo hafahamu lolote kuhusu hicho kinachoelezwa kutumia dawa za kulevya. 


Kikosi cha Yanga VS Azam FC

                                            Kikosi cha Yanga kitakachovaana na Azam FC leo

Kabila ataja mwezi wa kufanyika uchaguzi DR Congo

Rais Joseph Kabila amepinga ukosoaji unaotekelezwa na jamii ya kimataifa kuhusu kucheleweshwa kwa uchaguzi katika jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Katika mkutano na wanahabari kuadhimisha miaka 17 madarakani, aliahidi kwamba uchaguzi huo utafanyika mwisho wa mwaka huu.

Kulingana na mwandishi wa BBC Alex Duval Smith mkutano huo na vyombo vya habari mjini Kinshasa ulikuwa wa kwanza katika kipindi cha miaka mitano.Na ulichukua saa tatu.

Aliikosoa Monusco akisema ujumbe huo wa Umoja wa Mataifa hauko nchini DRC ili kuendesha shughuli za taifa hilo.

Katika shutuma dhidi ya muungano wa Ulaya na Marekani, ambao wamekosoa makabiliano dhidi ya waandamanaji, alisema: DRC sio koloni .Taifa hili lazima liheshimiwe.

Alionekana akilikumbusha kanisa katoliki akisema kuwa maandamano yanayofanywa na wakristo dhidi ya serikali yake yanafaa kuruhusiwa lakini waandalizi ni lazima washtakiwe.

Serikali hiyo hivi majuzi ilitangaza kwamba uchaguzi utafanyika tarehe 23 Disemba, ikiwa ni miaka miwili baada ya kukamilika kwa muda wa utawala wa rais huyo.

Kampuni ya Mugabe yaingia kwenye matatizo

Kampuni moja ya rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe inatakiwa kuondoka katika kipade kimoja cha ardhi kinachomilikiwa na shule moja la sivyo ishtakiwe.

Kampuni hiyo kwa Jina Gushungu Holdings inadaiwa kunyakuwa kipande hicho cha ardhi chenye ukubwa wa hekari 23 katika eneo moja la makaazi ya mji wa Harare.

Kanisa la Reform linasema kuwa ardhi hiyo inamilikiwa na kundi la shule zake la Eaglesvale.

Wakili wa shule hiyo Rodney Makausi aliambia BBC kwamba mwaka 2016 serikali ilichukua ardhi hiyo kwa nguvu.

Serikali baadaye ikaondoa madai yake baada ya swala hilo kuwasilishwa mahakamani.

Lakini mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo Enos Chomutiri anasema kuwa mahindi yalipandwa katika shamba hilo mwaka uliopita na bango kubwa la shule hiyo likaondolewa.

Mawakili wametaka kampuni hiyo kuondoka katika shamba hilo mwisho wa mwezi huu ama ishtakiwe.

Sio mara ya kwanza familia ya Mugabe imetuhumiwa kuchukua mali kwa nguvu.

Awali, familia hiyo imekuwa na mgogoro na wakulima masikini kuhusu ardhi moja inayodaiwa kuwa na utajiri wa dhahabu ,pia familia hiyo imetuhumiwa kwa kunyakua shamba moja linalalozalisha ndimu zinazouzwa nje ya taifa katika eneo hilo hilo.

Bodi ya Ligi yaipiga rungu Mbeya City

Timu ya Mbeya City

Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania kupitia Mkurugenzi wa Ligi Boniface Wambura imetangaza kuipiga faini ya jumla ya shilingi milioni moja klabu ya Mbeya City kwa makosa mawili tofauti.

Wambura amebainisha hayo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam na kusema timu hiyo ilitenda kosa la kutumia mlango usio rasmi kuingilia uwanjani katika mechi iliyofanyika Januari 1,2018 Jijini Mbeya ambapo kitendo hicho ni kosa kwa mujibu wa kanuni za ligi kuu na kutozwa laki 5 kama adhabu yao.

Aidha, Wambura alisema Kamati iliiagiza Sekretarieti ya Bodi ya Ligi kutoa waraka kwa wamiliki wa viwanja kuhakikisha timu zote zinaingia uwanjani kwa kutumia milango rasmi nasio vinginevyo.

Mbali na hilo, Wambura amesema Klabu hiyo pia imepigwa faini ya laki 5 kutokana na mashabiki wake kuingia uwanjani na kumzonga mwamuzi kwa madai alikataa kutoa 'penalti' kwa timu hiyo.

Kwa upande mwingine, Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania kupitia Mkurugenzi wa Ligi Boniface Wambura imetangaza kumfungia kocha wa timu hiyo Ramadhani Mwazurimo mechi mbili na kupigwa faini ya laki 5 kutokana na kutoa lugha ya kashfa katika mechi ya Tanzania Prisons dhidi ya Mbeya City iliyochezwa Januari 14, 2018 kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Lowassa amnadi Salum Mwalimu Kinondoni

Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu wa Chama cha Demokrasia na  Maendeleo CHADEMA, Edward Lowassa jioni leo amemnadi Mgombea wa Ubunge wa Kinondoni kupitia chama hicho, Salumu Mwalimu huku akiwataka wakazi wa Kinondoni kuacha kumuongelea mgombea wa CCM, Maulid Mtulia maana amekuwa msaliti kwao.

Lowassa alitumia wakati huo pia kuwashukuru wananchi wa Kinondoni kwa kumpigia kura wakati wa uchaguzi mkuu uliopita, na kuwaomba zile kura walizompigia 2015 basi wazielekeze kwa Mwalimu ambaye anaamini ni msomi mwenye kuweza kuwatetea wakazi wa Kinondoni.

" Msiogope vijana wa Kinondoni wenzetu wamekuwa wajanja wakilinda kura zao sasa na sisi kama ambavyo wazungumzaji wengine wamesema basi tunaomba mlinde kura zetu ikiwezekana tulale katika vituo vya kupigia kura kuhakikisha hatuibiwi.

Nae Waziri Mkuu Mstaafu wa awamu ya tatu, Fredrick Sumaye alisem, " Hakikisheni mnamchagua Mwalimu huyu ndie mtu safi wa kuhakikisha analeta maendeleo katika jimbo lenu,"

Kwa upande wake Mwalimu ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, alisema " Achaneni na wao wanaosema mimi sio mkazi wa hapa nachoomba ni kura zenu ambazo zitanifanya nikawatetee kuwajengea shule, kuhakikisha ajira kwa vijana,"

Kampeni za chama hicho zitaendelea kesho katika eneo la Kigogo jijiji Dar es Salaam ambapo zitaongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe.

Taliban watumia 'ambulance' iliojaa vilipuzi kuwaua watu 95 Afghanistan

Mlipuaji wa kujitolea mhanga amewaua takriban watu 95 na kuwajeruhi wengine 158 katika mji mkuu wa wa Afghanistan Kabul, kulingana na maafisa.

Washambuliaji waliendesha ambyulensi iliokuwa imejaa vilipuzi kupitia kizuiazi cha polisi hadi katika barabara ambayo ilikuwa imetengewa wafanyikazi wa serikali.

Kisa hicho kilitokea katika jumba la wizara ya maswala ya ndani na afisi ya Muungano wa Ulaya na baraza kuu la amani.

Kundi la wapiganaji wa Taliban linasema kuwa walitekeleza shambulio hilo ambalo ni baya zaidi katika kipindi cha mwezi mmoja.

Walioshuhudia wanasema eneo hilo ambalo lina majumba ya balozi nyingi pamoja na makao makuu ya polisi mjini humo, lilikuwa na watu wengi wakati bomu hilo lilipolipuka siku ya Jumamosi .

Maafisa wanasema kuwa idadi ya waliofariki inaendelea kuongezeka huku majeruhi wakipelekwa hospitalini kwa matibabu.
Shirika la kimataifa la msalaba mwekundi limesema kuwa utumizi wa 'ambulence' unakera.Wiki moja iliopita ,wapiganaji wa Taliban waliwaua watu 22 katika hoteli moja ya kifarahari mjini Kabul.

Hili ndilo shambulizi baya zaidi kuwahi kufanyika mjini Kabul katika kipindi cha miezi kadhaa.

Mnamo mwezi Oktoba, watu 176 waliuawa katika shambulio la bomu mjini Afghanistan katika kipindi cha wiki moja.

Vikosi vya maafisa wa usalama vya Afghanistan vimeshambiliwa pakubwa na wapiganaji wa Taliban ambao wanataka kuweka sheria ya kiislamu katika taifa hilo.

Mnamo mwezi Mei, takriban watu 150 waliuawa na mpiganaji wa kujitolea mhanga mjini Kabul.

Kundi la wapiganaji wa Taliban walikana kutekeleza shambulio hilo lakini serikali ya Afghanistan inasema kuwa kundi la Haqqani ambalo ni mshirika wake lilitekeleza shambulio hilo kupitia usaidizi wa Pakistan.

Pakistan imekana kusaidia kundi lolote la wapiganaji linalotekeleza mashambulizi nchini Afghanistan .

Mwezi huu, Marekani ilikatiza usaidizi wake wa usalama kwa Pakistan, ikisema kuwa taifa hilo limeshindwa kuchukua hatua dhidi ya makunni ya kigaidi katika ardhi yake.


Matapeli wa Viwanja DSM kukiona

Serikali ya Mkoa wa Dsm Imetangaza rasmi vita dhidi ya Matapeli wa Viwanja na Nyumba ambao wamekuwa wakitumia mbinu mbali mbali ikiwemo ofisi za mawakili ,mahakama pamoja na Madalali kuwadhulumu wajane pamoja na watu wasiokuwa na Uwezo.

Mkuu wa Mkoa wa Dsm Paul makonda akizungumza na waandishi wa habari baada ya kwenda kwa familia ya Bi,Stella Bejumula pamoja Mume wake ambao ni watumishi wastaafu wa serikali ambao wametapeliwa nyumba kwa zaidi ya Miaka sita na kuishi maisha ya Kutangatanga na kutegemea Misaada ikiwemo chakula kutoka kwa watu mbali mbali..

Aidha Familia hiyo ya Bejumula ilitoa mtiririko mzima wa kadhia ya Kutapeliwa ambapo mwaka 2012 walikopa bank ya Crdb Mkopo na kufanikiwa kurejesha zaidi ya asilimia 80,na kubaki million ishirini ambayo alitokea Mtu mmoja kuwakopesha kwa riba lakini baadae akadaiwa kutengeneza Mkataba bandia wa mauzo kuwa familia hiyo imemuuzia kwa milion 96 Huku nyumba hiyo ikiuzwa kwa mtu mwingine katika kipindi cha siku 4 tu baada ya deni kulipwa.

Aidha Makonda alikwenda katika nyumba iliyopo kitalu B namba 91 ambayo ilikuwa ikimilikiwa na mzee na Bi,Bejumula na kutoa agizo la mmiliki aliyeuziwa eneo hilo kufika ktika ofisi za Mkuu wa Mkoa na nyaraka alizofanikisha kununua eneo hilo.

Makonda pia aliwakabidhi wazee hao wastaafu vyakula mbali mbali ikiwemo,Mchele,mafuta,unga, ngano na sukali huku akimtaka mfadhili anayewasaidia malazi aendelee kuwasaidia wakati akishughulikia suala hilo hali iliyozua simanzi eneo hilo …

Yanga SC yavunja rekodi ya Azam FC Chamazi

Mchezo wa ligi kuu soka Tanzania Bara baina ya mabingwa watetezi klabu ya Yanga dhidi ya Azam FC umemalizika katika uwanja wa Azam Complex Chamazi kwa mabingwa hao kushinda jumla ya mabao 2-0.

Kwa ushindi wa Yanga SC unaifanya timu hiyo kuvunja rekodi ya wana lamba lamba Azam FC ya kutokupoteza hata mchezo mmoja toka kuanza kwa ligi kuu soka Tanzania Bara msimu huu wa mwaka 2017/18.

Wafungaji katika mchezo alikuwa Shabani Chilunda wa Azam FC wakati kwa upande wa Yanga SC akiwa Obrey Chirwa na Gadiel Michael.

Kwa matokeo hayo inaifanya mabingwa watetezi Yanga SC kufikisha jumla ya pointi 28 wakiwa nafasi ya tatu, Azam FC ikisalia na alama zake 30 nafasi ya pili huku Simba SC ikiongo katika msimamo wa ligi kwa kuwa na pointi 32 na mchezo mmoja mkononi ambao unatarajiwa kupigwa hapo kesho siku ya Jumapili.

Katika michezo mingine iliyopigwa hii leo timu ya Mbeya City ikiwa nyumbani imekubali kutoka sare ya mabao 0 – 0 dhidi ya Mtibwa Sugar wakati Mwadui FC ikiwa nyumbani imelizimishwa sare ya magoli 2 – 2 na Njombe Mji wakati Kagera Sugar ikitoka suluhu ya bila kufungana dhidi ya Lipuli FC.

Mtulia kuweka hadharani mikakati yake Kinondoni

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa CCM Wilaya wa Kinondoni, Harold Maruma amesema mgombea ubunge wa Kinondoni kwa tiketi ya chama hicho, Maulid Mtulia atatumia uzinduzi wa kampeni kueleza mikakati yake ya kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

CCM inazindua kampeni leo Jumamosi Januari 27,2018 kuanzia saa 10:00 jioni katika viwanja vya Biafra jijini Dar es Salaam.

Maruma amesema baadhi ya changamoto zitakazozungumzwa na mgombea huyo ni barabara na mikopo kwa akina mama.

"Tunaomba wakazi wa Kinondoni kujitokeza  kwa wingi na Jeshi la Polisi limetuhakikishia kuwa hakuna mtu atakayedhurika wakati wa kampeni na wakati wa kurudi nyumbani," amesema.

Wengine wanaoshiriki uzinduzi wa kampeni hizo ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Kate Kamba na wabunge wake wa mkoa wa Dar es Salaam.

Tayari viongozi wakuu wa chama hicho tawala waliofika katika uwanja wa Biafra wametambulishwa na kuipisha bendi ya bendi ya TOT inayotoa burudani ya nyimbo za  kuhamasisha wana CCM.

Watu 30 Wapoteza Maisha Katika ajali ya moto Korea Kusini

Imethibitika zaidi ya watu 30 wamekufa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika ajali ya moto uliotokea katika Hospitali moja nchini Korea Kusini.

Hata hivyo maafisa wa nchi hiyo wanasema idadi ya waliokufa huenda ikaongezeka kutokana na baadhi ya watu kujeruhiwa vibaya.

Imefahamika kuwa moto huo ulianzia katika chumba cha dharura cha Hospitali ya Sejong, kusini mashariki mwa nchi hiyo.

Zaidi ya majeruhi 100 wanasemekana wamo katika jengo la hospitali hiyo.

Mwaka jana watu 29 walikufa katika mji wa Echeon, Korea Kusini, na wengine kujeruhiwa baada ya moto kuzuka katika sehemu ya mazoezi ya wazi.

VIDEO: Makonda Aangua Kilio


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda  leo ametembelea na kutoa pole  kwa Familia ya Wastaafu ya Bwana Edward Bejumula na Bi. Stella Bejumula walioteseka kwa Miaka Sita bila Makazi baada ya kudhulumiwa Nyumba yao ambapo ameahidi kulivalia njuga suala hilo kuhakikisha haki inatendeka bila kuvunja sheria.

 TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI .....USISAHAU KUSUBSCRIBE



VIDEO: Full Video CCM Wakizindua Kampeni Kinondoni


Chama cha Mapinduzi CCM kimezindua kampeni zake za Ubunge wa jimbo la Kinondoni huku Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba pamoja na Waziri wa zamani wa Maji, Steven Wassira wakimnadi mgombea wa Chama hicho, Maulid Mtulia.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI...USISAHAU KUSUBSCRIBE