Monday, 4 December 2017

Marekani yatakiwa isiutambue Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel



Ayman Safadi alisema alimuambia waziri wa mashauri wa nchi za kigeni wa Marekani Rex Tillerson kuwa hatua kama hiyo inaweza kuzua ghadhabu kubwa kwa nchi za kiarabu na ulimwengu wa kiisalmu.

Kuna uvumi kuwa Rais Donald Trump atatangaza hilo hivi karibuni na kutimiza ahadi yake aliyotoa wakati wa kampeni.

Jared Kushner, mkwe wa Trump alisema kuwa bado hakuna uamuzi uliofanywa.

Ubalozi wa Marekani kuhamia Jerusalem?

Palestina: Uhamisho wa ubalozi utaathiri amani

Katika mtandao wa Twitter, Bw Safadi alisema: #Nilizungumza na waziri Rex Tillerson kuhusu hatari ya kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.

Hatua kama hiyo inaweza kusababisha ghadhabu kwenye nchi za kiarabu na kwa ulimwengi wa kiislamu na kuzua misukosuko na pia kuhujumu jitihada za amani."

Kuna uvumi kuwa Rais Donald Trump atatangaza hilo hivi karibuni na kutimiza ahadi yake aliyotoa wakati wa kampeni.

Hakuna jibu lolote kutoka kwa wizara ya mashauri ya nchi za kigeni nchini Marekani.

Naye rais wa Palestina Mahmoud Abbas anajaribu kupata uungwaji mkono wa kimataifa katika kumshawishi Trump asifanye tangazo kama hilo.

Ofisi yake ilisema kwa aliwapigia simu Jumapili viongozi wa dunia wakiwemo rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan.

Askofu aliyewapatia silaha Wapalestina dhidi ya Israel afariki

"Alitaka kulezea harari za uamuzi wowote wa kuhamisha ubalozo wa Marekani kwenda Jerusalem au kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Isael," mshauri wa Bw. Abbas, Majdi al-Khalidi aliliambia shirika la AFP.Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni nchini Jardan ameonya Marekani kuhusu hatari ya kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.

Polepole amesema Chama chake hakitampokea Mtu adi afuate taratibu



Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole  amesema Chama cha Mapinduzi (CCM) hakitampokea yeyote anayetaka kurudi ndani ya chama hicho bila kufuata utaratibu. Kauli hiyo imekuja baada ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kinondoni(CUF), Maulid Said Abdallah Mtulia kutangaza kujiuzulu nafasi zake zote za uongozi alizokuwa akizishikilia kwenda CCM

Polepole aliyasema hayo wakati akiwahutubia wananchi wa CCM mkoa wa Mara katika uchaguzi wa Mwenyekiti wa Mkoa wa Chama.

“Ameamua kule aliko haoni itikadi,haoni siasa, haoni mwelekeo, Chama kina baba wawili huwezi kuwa na nyumba ina baba wawili alafu utasikiliza watoto watamsikiliza nani, basi amehama,” alisema Polepole.

“Sasa mimi niko hapa Musoma mimi nitumie fursa hii anayemuunga mkono ni Rais wetu ambaye ni mwana CCM kwelikweli na ndiye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi ikimpendeza afuate utaratibu akiona mazuri ya Rais yule asione vinaelea kwa mazuri yale asione vimeshushwa vimeundwa na wanaounda mambo mazuri ya Magufuli ni Chama cha Mapinduzi.

Audio | Young Dee Ft Dayna Nyange _ Ki Ben Ten | Mp3 Download

Audio | Young Dee Ft Dayna Nyange _ Ki Ben Ten | Mp3 Download

Audio | Young Dee Ft Dayna Nyange _ Ki Ben Ten | Mp3 Download

                 DOWNLOAD NOW

Diamond Platnumz aomba radhi kwa wanachuo,,,

Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz jana alikuwa kwenye orodha ya wasanii wa WCB ambao walitakiwa kutumbuiza kwenye Party maalumu ya kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Vyuo vikuu vilivyopo Dar es salaam lakini cha ajabu hakutokea jukwaani.
Sasa leo kupitia ukurasa wake wa Instagram Diamond Platnumz amewaomba radhi mashabiki wake kwa kutotokea kwenye party hiyo ya Dar Freshers ambayo iliandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Mhe. Paul Makonda kwa kusema kuwa, hata yeye alikuwa na hamu ya kujumuika na vijana wenzake lakini haikuwa riziki kwake.
Najua wengi mlikuwa na Shauku kubwa ya uwepo wangu pale Mlimani City jana ila amini kuwa, shauku yangu ya kuwepo pale kuimba na kufurahi pamoja nanyi, ilikuwa ni kubwa kuliko yenu na ndiomaana nilijitahidi sana kuhamasisha kwa uwezo wangu wote ili kwa wingi tufike pale….lakini kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wangu sikuweza kufanikiwa kufika. Pengine Haikuwa Riziki yangu ama Labda Mwenyezi Mungu hakuniandikia siku ya jana kujumuika nanyi pale. Hivyo tusisononeke wala kuchukia…Niwaombe radhi na kuwapa pole wote ambao waliokwazika jana…Inshaallah Mwenyez Mungu siku akiniandikia kuwa pamoja nanyi ntawataarifu….. nimpongeze pia Mkuu wa mkoa pamoja na waandaaji wote, Wanavyuo, Media , na wasanii wote kwa kuifanikisha #FreshersParty. Hakika Historia iliandikwa🔥🔥🔥
Dar Freshers Party ilifanyika jana katika ukumbi wa Mlimani City na ilitumbuizwa na wasanii kutoka WCB, na wengine ni Dully Sykes, Ray C, Lady JayDee, Ruby, Christian Bella, Fid Q na Mwana FA.

Saturday, 2 December 2017

Audio | Nay Wa Mitego Ft Billnas X Godzilla X Ay – Muda Wetu Remix.| Mp3 Download

Audio | Nay Wa Mitego Ft Billnas X Godzilla X Ay – Muda Wetu Remix.| Mp3 Download

Audio | Nay Wa Mitego Ft Billnas X Godzilla X Ay – Muda Wetu Remix.| Mp3 Download


                                       DOWNLOAD HERE

Ratiba kombe la Dunia yatoka, Misri yakabidhiwa wenyewji



Nigeria wamepangwa kwenye kundi moja na Argentina kwa mara nyingine, Misri nao wakapangwa na Urusi na Uruguay baada ya droo ya Kombe la Dunia 2018 kufanywa nchini Urusi.

Panama, ambao wanacheza Kombe la Dunia mara ya kwanza wamepangwa na Ubelgiji na England na Tunisia.

Iceland, walioshangaza wengi kwa kufuzu, wamepangwa kucheza na Nigeria, Croatia na Argentina katika Kundi D.

Mechi ya ufunguzi itakuwa kati ya Urusi na Saudi Arabia.

Droo kamili ya Kombe la Dunia:

Kundi A: Urusi, Saudi Arabia, Misri, Uruguay
Kundi B: Ureno, Uhispania, Morocco, Iran
Kundi C: Ufaransa, Australia, Peru, Denmark
Kundi D: Argentina, Croatia, Iceland, Nigeria
Kundi E: Brazil, Uswizi, Costa Rica, Serbia
Kundi F: Ujerumani , Mexico, Sweden, Korea Kusini
Kundi G: Ubelgiji , Panama, Tunisia, England
Kundi H: Poland, Senegal, Colombia, Japan.


Fifa wamepokea maombi 3.5 milioni ya tiketi, 300,000 yakiwa maombi ya tiketi za mechi ya fainali uwanjani Luzhniki.

Asilimia 57 ya maombi yametoka kwa wakazi wa nje ya Urusi. Tiketi ya bei nafuu zaidi ya fainali Kombe la Dunia ambayo raia asiye wa Urusi anaweza kununua ni ya £345.

Kombe la Shirikisho kuanza kutimua vumbi Desemba 22




Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa sasa itasimama kwa takribani majuma mawili sababu kubwa ni kupisha Kombe la Chalenji la CECAFA michuano inayoratibiwa na Baraza la Soka kwa nchi za Afrika Mashariki (CECAFA).

Kutokana na michuano hiyo kuingilia ratiba, kwa mujibu wa Shirikisho la soka nchini (TFF), Desemba 22, 23, 24 na 26, zitakuwa siku za mechi za kuwania Kombe la Shirikisho la Azam yaani Azam Sports Federation Cup (ASFC).

Mechi zitakazochezwa katika siku hizo zitafahamika Desemba 5, mwaka huu ambako imepangwa droo ya timu 64 zitakazocheza Raundi ya Tatu ya ASFC.

Timu 64 maana yake ni kuwa timu 16 za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara; timu 24 za Ligi Daraja la Kwanza na timu 24 ambazo zimefuzu kutoka hatua awali; ya kwanza na pili.

Baada ya michezo hiyo, ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom itaendelea tena kwa michezo ya raundi ya 12 itakayofanyika Desemba 29, 30 na 31 kabla ya ligi tena kusimama kupisha michuano ya Kombe la Mapinduzi.

Michuano ya CECAFA itafikia ukomo Desemba 17, mwaka huu na Shirikisho

Mbao FC waitwa mezani na Mshambuliaji wa Stand


Wakati Mbao FC ikiwa na tatizo katika safu ya ushambuliaji, mshambuliaji wa Stand United, Omary Kanyoro amesema yupo huru kuzungumza na timu yoyote inayotaka huduma yake.

Mbao imekuwa na tatizo katika safu ya ushambuliaji ambayo imekuwa ikikosa mabao ya wazi katika msimu huu wa Ligi Kuu.

Kanyoro alisema kwa sasa yuko huru kujiunga na klabu yoyote kwani msimu huu hakusajili Stand United katika dirisha kubwa la usajili.

Alisema anatamani kuchezea klabu ya Mbao ambayo katika msimu wa 2016/17 alitaka kusajiliwa, lakini Stand United wakapanda dau kuwazidi wachana Mbao hao wa jiji la Mwanza.

“Mbao ni timu nzuri na kwa sasa natamani kwenda kuchezea kwani ina kocha mzuri hivyo kama wakija basi nipo tayari kujiunga nao”alisema Kanyoro.

Hata hivyo Mshambuliaji huyo alisema pia anakaribisha ofa kwa klabu mbalimbali za Ligi Kuu na Daraja la Kwanza ambapo yeye yuko tayari kukipiga iwapo watahafikiana kwenye maslahi.

“Sikuweza kusaini mkataba mpya na Stand United katika dirisha kubwa la usajili kutokana na sababu mbalimbali lakini kwa sasa niko huru hivyo klabu yoyote nakaribisha ofa zao,”alisema mshambuliaji huyo.

Chege afananisha ustaa na Jela



Msanii wa Bongo Flava, Chege amesema msanii kuwa staa ni sawa na jela.

Muimbaji huyo wa ngoma ‘Run Town’ ameiambia 5 Selekt ya EATV kuwa kwa wale wasiofahamu wanaweza kuchukulia hilo kawaida lakini ukishakuwa staa ndio utagundua hilo.

“Mtu unapokuwa unaangaika kutafuta ustaa lakini ustaa ni jela moja mbaya sana kwa mtu ambaye hajawahi kupitia hiyo kitu anaweza akaona huyu anaongea tu lakini ukishakua pale kwenye ustaa ndio unajua majukumu ya ustaa yakoje” amesema.

Chege amepongeza kuwa hilo halijamsumbua kwani toka awali alikuwa kwenye mafunzo ya kuupokea ustaa na alikaa na mastaa kwa muda mrefu kabla hajawa staa.

“Siyo kukaa nao tu na kukutana masikani, no! nilikua ndani ya kundi ambalo lina staa namba moja Tanzania nzima kwa hiyo hadi nakuja kuwa staa ule ushamba wa ustaa siwezi kuwa nao tena” amesema Chege.

Adhabu kutolewa kwa wanaosema uongo



Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa amewaonya baadhi ya watu wanaoendelea kutoa takwimu za uongo ambazo husababisha taifa kuingia kwenye mvutano na nchi wahisani wa maendeleo kwa kuogopa kusaidia wananchi.

Dkt. Chuwa amesema moja ya changamoto wanayokutana nayo katika ofisi yake na wadau wa maendeleo, ni baadhi ya takwimu kuonyesha ukubwa wa tatizo kwa kiwango ambacho hakijafikiwa, na kuleta hofu kwa wadau hao hali ambayo inasababisha taifa kukosa ushirikiano mzuri na nchi zingine, kwa kuogopa kusaidia taifa lenye nguvu kazi ya kusuasua.

Kutokana na hilo Mkurugenzi huyo anayesimamia masuala ya takwimu, ameagiza watendaji wake kuhakikisha wanawachukulia hatua za kisheria wale wote watakaobainika kutoa takwimu za uongo, na kuliingiza taifa katika hali ya sintofahamu.

Kwa upande mwengine baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wameiomba jamii kuacha kusambaza takwimu za uongo, na kuziachia mamlaka husika za serikali kutekeleza jukumu hilo la utoaji wa takwimu zilizosahihi.

Guardiola hajutii kuongea na Redmond


Meneja wa Manchester City Pep Guardiola amesema anajutia sana mazungumzo ambayo alifanya na mchezaji wa Southampton Nathan Redmond punde baada ya mechi yao kumalizika Jumatano.
City walishinda 2-1.

Guardiola, ambaye aliingia uwanjani na kuzungumza na winga huyo, ametakiwa kufafanua kuhusu kitendo hicho chake na Chama cha Soka cha England.

Redmond amesema Mhispania huyo alikuwa tu anamsifia.

Ijumaa, Guardiola alisema: "Siwezi kujidhibiti. Natumai nitaweza kufanya hivyo, natumai naweza kuimarika."

Meneja huyo wa zamani wa Barcelona na Bayern Munich amepewa hadi Jumatatu kutoa ufafanuzi.
"Kile Redmond alichosema ndicho hicho, navutiwa naye kama mchezaji na namshukuru kwa aliyoyasema," amesema.

"Iwapo FA wanataka taarifa yangu tena, ninaweza kufafanua chochote wanachotaka nifafanue. Ikiwa hawaniamini, sijui nafanya nini hapa."

Guardiola alimwendea Redmond muda baada ya Raheem Sterling kufunga bao la ushindi la City dakika ya 96 uwanjani Etihad.

Alianza kusema kwa sauti na kuashiria kwa mikono yake, huku Redmond akionekana kufunika mdomo wake na kumjibu.

Redmond baadaye amesema: "Nilimwambia kwamba nilikuwa ninafanya kile nilichoambiwa na meneja wangu kufanya kwenye mechi hiyo. Hivyo tu."

City watakuwa wenyeji wa West Ham saa 16:00 Jumapili nao Southampton watakuwa ugenini dhidi ya Bournemouth saa 13:30 siku hiyo.



Diamond adaiwa kumkacha Ali Kiba


Muimbaji Diamond Platnumz wiki hii baada ya kuachia nyimbo mbili, Sikomi na Niache, aliahidi Ijumaa hii kuachia rasmi wimbo wake mpya uitwao ‘Waka’.

Meneja wa nyota huyo, Sallam SK amewaomba radhi mashabiki wa muimbaji huyo mwenye tuzo nyingi za kimataifa kwa madai kuna dharura imetokea hivyo atashindwa kuachia project hiyo inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa muziki.

“Tunaomba msamaha wimbo wa ‘Waka’ ulitakuwa kutoka siku ya leo kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu kwahiyo hautaweza kutoka leo lakini muda sio mrefu tutawajuza!! Sorry for any inconvenience,” aliandika meneja huyo.

Wadau wa mambo wamedai muimbaji huyo ameshindwa kuachia kazi hiyo mpya ili kuepusha kazi hiyo kushindanishwa na wimbo mpya wa msanii wa RockStar4000, Alikiba, ‘Maumivu Per Day’.

Hata hivyo mashabiki wa Diamond wameonyesha kuchukizwa vikali na uamuzi huo huku wengine wakiwa na maoni tofauti.

Mark Hughes aponda kiwango cha Atkinson



Meneja wa klabu ya Stoke City Mark Hughes amesema Martin Atkinson hafai kutumiwa kama mwamuzi mechi za Ligi ya Premia msimu huu baada ya kufanya "kosa kubwa" mechi za katikati ya wiki.

Atkinson alimpa mlindalango wa Liverpool Simon Mignolet kandi ya manjano pekee kwa kumwangusha mshambuliaji wa Stoke Mame Diouf, akiwa ndiye mchezaji wa mwisho Jumatano.
Stoke walikuwa 1-0 chini wakati huo.

Walishindwa 3-0 mwishowe na Hughes alisema "kila mtu alijua" hiyo ilifaa kuwa kadi nyekundu.
"Sioni ni kwa nini anafaa kusimamia mechi wikendi hii," aliongeza.

"Hisia zangu ni sawa na za kila mtu: waamuzi ambao walitazama tena kisa hicho na kila mtu uwanjani, kando na mmoja pekee.

"Kuna maamuzi yanayoniuma sana mimi kama meneja - na mameneja wengine.

"Sababu ya hiyo kutokuwa (kadi nyekundu) mimi sijui. Ulikuwa uamuzi rahisi sana kwangu lakini haukufanywa. Hilo lilitunyima fursa ya kujipatia nafuu. Nimekasirishwa sana na hilo."

Atkinson atasimamia mechi ya Watford nyumbani dhidi ya Tottenham Ligi ya Premia Jumamosi.

Aprili 2016, Bodi ya Kimataifa vya Soka (IFAB) iliidhinisha kubadilishwa kwa kanuni za soka na kuondoa hitaji la kadi nyekundu moja kwa moja kwa mchezaji anayefanya kosa linalomnyima mpinzani nafasi wazi ya kufunga bao.