Monday, 16 October 2017

Waziri Mkuchika kupeleka ombi Bungeni umri wa kustaafu uongezwe

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema anakusudia kupeleka ombi maalum Bungeni kuomba umri wa kustaafu kwa Maprofesa uongezwe na kufikia 65 badala ya 55.
Waziri Mkuchika ameyasema hayo alipokwenda alipotembelea ofisi za Sekretarieti ya Ajira na kukutana na watendaji wa taasisi hiyo, na kusema kwamba umri wa kustaafu kwa sheria unawafanya wasomi hao washindwe kutumika vizuri kulijenga Taifa.
"Hawa maprofesa wengi wanaofikia hatua hiyo wanakuwa na miaka kuanzia 50 na kuendelea, halafu anafanya kazi kidogo anatakiwa kustaafu, tutapeleka bungeni maombi kuwe na mabadiliko kidogo katika baadhi ya maeneo, haitakuwa na maana kama wasomi wanatumia rasilimali za taifa kufikia hatua hiyo halafu baada ya kuhitimu wanafanya kazi kwa muda mfupi na kutakiwa kustaafu", amesema Waziri Mkuchika.
Katika ziara hiyo Waziri Mkuchika ameahidi kushughulikia changamoto zinazoikabili sekta hiyo, ikiwemo sheria na utaratibu wa ajira unaopitia kwenye Sekretarieti ya ajira.

Pogba Aanza kujinoa,,,,


Diamond Afunguka kuhusu pochi ya Zari

Baada ya Zari kuonekana kwenye uzinduzi wa duka la vifaa vya nyumbani na Ofisini Danube Mlimani City baadhi ya mitandao na watu walianza kusema kwamba amebeba pochi ya bei rahisi, hilo limemfikia mpaka Diamond na akaamua kusema yafuatayo.
Diamond amezima taarifa hizo kwa kusema pochi hiyo alimnunulia Zari shilingi milioni 5 za Kitanzania hivyo haitakiwi kushushwa thamani.

Gigy money atangaza dau lake,,,,,

Msanii wa Bongo Fleva na Video Queen, Gigy Money amesema kwa sasa kama promota au mtu yeyote anayehitaji kumuita kutumbuiza kwenye tamasha/sherehe yake basi ni lazima uwe na kiasi cha milioni mbili za kitanzania.
Mkali huyo anayetamba kwa sasa na wimbo wake wa ‘Papa’ amesema wimbo huo ni ‘Hit Song’ na ni moja ya wimbo mkali kwa sasa kuliko nyimbo nyingine zilizotoka kwa muda huu.
“Na-perform stejini kwa milioni mbili, Papa is a hit song, bila milioni 2 siwezi kutoa Papa stejini, is a hit song.“amesema Gigy Money kwenye mahojiano yake na Bongo5.

Waziri Mkuu Amewaonya Mawaziri,,,,,

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaonya mawaziri na kuwataka watumie madaraka yao kwa manufaa ya Taifa na kamwe wasiyatumie kama fursa ya kujitajirisha wao binafsi.
Kassim Majaliwa amesema hayo leo Oktoba 16, 2017 alipozungumza na baadhi ya Mawaziri, Manaibu na Makatibu Wakuu katika kikao kilichofanyika jijini Dar es Salaam. Aidha Waziri Mkuu amesema Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli amesisitiza kwamba amewateua ili wafanye kazi na kamwe wasitumie madaraka waliyopewa kwa maslahi yao binafsi.
“Madaraka haya ya Uwaziri si fursa ya kujipatia utajiri, tunatakiwa tufanye kazi kwa weledi, uadilifu, bidii na uaminifu mkubwa ili kuondoa kero za wananchi kwa wakati.”
Waziri Mkuu amesema Mawaziri hao wanatakiwa wasimamie utekelezaji wa mpango wa maendeleo wa Taifa wa miaka kuanzia mwaka 2016/2017 hadi 2020/2021. Pia utekelezaji wa ahadi zote zilizopo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 pamoja na ahadi alizozitoa Rais Dkt Magufuli wakati wa kampeni za uchaguzi.
Hata hivyo Waziri Mkuu amewataka Mawaziri hao wakapunguze urasimu katika utekelezaji wa malengo ya Serikali kwa sababu wananchi wanahitaji kuhudumiwa kwa wakati Mawaziri waliohudhuria kikao hicho ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais –TAMISEMI Bw. Suileiman Jaffo pamoja na Manaibu wake Bw. Joseph Kandege na Bw. George Kakunda, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi Ummy Mwalimu na Naibu wake Dkt. Faustine Ndungulile.
Wengine ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe na Naibu wake Bw. Jumaa Aweso, Waziri wa Viwanda na Biashara Bw. Charles Mwijabe na Naibu wake Mhandisi Stella Manyanya.
Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla na Naibu wake Bw. Josephat Hasunga, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako na Naibu wake Bw. William Ole Nasha, Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Bw. Abdallah Ulega pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara hizo.

Idadi ya watu waliouawa kwenye mlipuko mkubwa Wa mabomu Mogadishu yafika 300

Idadi ya watu waliouawa kwenye ,lipuk

o mkubwa wa bomu katika eneo lenye shughuli nyingi kwenye mji mkuu wa Somalia Mogadishu siku ya Jumamosi, imefikia watu 300 hadi sasa, kwa mujibu wa ripoti ya shirika la hahari la Reuters
Takriban watu wengine 300 walijeruhiwa kwa mujibu wa AFP, wakati lori lililokuwa limejazwa milipuko lilipolipuka karibu na lango la hoteli.
Reuters walimnukuu Ahmed Ali, muuguzi anayefanya kazi kwenye hospitali moja akisema kuwa miili 160 haikuweza kutambuliwa na hivyo ilizikwa na serikali jana. Anasema kuwa miili mingini iliziwa na jamaa zao,.
Hilo ndilo shambulizi baya zaidi kutokea nchini Somalia tangu kundi la al-Shabab lianzishe harakati zake mwaka 2007.
Rais Mohamed Abdullahi "Farmajo" Mohamed alilaumu kundi la al-Shabab kwa shambulizi hilo katili.
"Tumethibitisha kuwa watu 300 waliuawa kwenye mipuko huo. Idasi ya waliokufa huenda bado ikaongezeka na kuna watu kadha ambao bado hawajulikani waliko," Abdikadir Abdirahman, mkurugenzi wa idara ya magari ya kusafirisha wagonjwa aliliambia shiria la Reuters.

Rais Magufuri Apongezwa

Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana wa UVCCM Taifa Shaka Hamidu, amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli kwa kurejesha mwamko ndani ya chama.
Shaka amesema kuwa katika uongozi wa Rais Magufuli kama Mwenyekiti wa Chama cha CCM, UVCCM imeweka rekodi ya kupokea maombi mengi zaidi ya watu wanaowania nafasi ya Uenyekiti Taifa kwenye uchaguzi wa mwaka huu. Jumla ya vijana 113 kutoka Tanzania bara na Zanzibar wamejitokeza kuwania nafasi hiyo.
“Katika uongozi wa Dkt, Magufuli akiwa Mwenyekiti wa chama limekuwa ni jambo la historia inaonyesha jinsi gani vijana wamekuwa na mwamko na hamu ya kukitumikia chama, kwakweli anastahili pongezi na hizi ni dalili nzuri kwa Chama”, amesema Shaka.
Kwa upande mwingine Shaka amesema hivi sasa zoezi linaloendelea ni usaili wa wagombea wote walioonesha nia ya kuwania uongozi ili kuwabaini na kuwapitisha wenye sifa sitahiki. Moja ya sifa kuu ya kugombea uongozi ndani ya UVCCM ni kuwa na miaka 30 au chini ya hapo ili katika uongozi wako usizidi miaka 35 kwani kila awamu ni miaka mitano.
Nafasi zinazowaniwa katika uchaguzi huo ambao mchakato wake umeanza tangu mwezi April kwa ngazi za Shina na Tawi ni Mwenyekiti, na Makamu wake, Wajumbe watano wa Halmashauri kuu ya Taifa (NEC), wajumbe watano wa baraza kuu la umoja huo Taifa na wawakilisha wa Jumuiya hiyo katika Jumuiya nyingine ndani ya chama.

Ibrahim Ajib Namba 10 Amekuja yanga wakati muafaka,,,

WAKATI mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara, Yanga SC walipoichapa KageraSugar FC 2-1 katika uwanja wa Kaitaba, Bukoba Jumamosi iliyopita na ‘kufunga’ gepu la pointi na viongozi wa ligi, kiungo-mshambulizi, Ibrahim Ajib ameendelea kuwathibitishia mashabiki wa klabu hiyo kuwa hahitaji sana muda ili kuanza kuwaonyesha ‘thamani’ yake.
Yanga ilikuwa timu pekee kati ya 16 kupata ushindi katika michezo ya mzunguko ya sita na alama hizo tatu walizozipata ugenini zimewafanya kufikisha pointi 12 sawa na Simba SC, Mtibwa Sugar FC na Azam FC ambao wote walishindwa kupata ushindi wakati michezo saba ya raundi hiyo ilipomalizika kwa matokeo ya sare/suluhu.
Magoli matatu ya Ajib, pointi 9 za Yanga
Yanga imeangusha pointi mbili tu katika michezo mitatu waliyocheza ugenini hadi sasa. Wamefanikiwa kufunga katika viwanja vya Sabasaba, Njombe (goli moja), Majimaji, Songea (goli moja) na wikendi iliyopita walipandisha kiwango chao kiufungaji kwa mara ya kwanza msimu huu walipofanikiwa kutikisa nyavu za golikipa Juma Kaseja mara mbili.
Ajib amehusika katika magoli matatu kati ya manne ambayo timu yake imefunga ugenini, huku akiongoza chati ya ufungaji katika kikosi hicho cha kocha Mzambia, George Lwandamina akiwa na magoli matatu kati ya sita ambayo timu yake imefanikiwa kufunga katika michezo sita iliyopita katika VPL.
Alifunga goli lake la kwanza akiwa mchezaji wa Yanga na kuisaidia timu yake kushinda 1-0 dhidi ya Njombe Mji FC. Goli hilo ni la kwanza la mpira uliokufa msimu huu. Akafunga tena katika ushindi wa 1-0 vs Ndanda FC katika uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Na sasa ametoka kufunga goli lake la tatu katika michezo sita ya ligi kuu, huku akipiga pasi ‘ya video’ kwa Obrey Chirwa aliyefunga goli la kwanza vs Kagera Sugar.
Hadi sasa Ajib amekuwa na mchango mkubwa sana katika kikosi cha Yanga hasa wakati huu ambao safu yao ya mashambulizi inatetereka kutokana na majeraha ya mara kwa mara yanayowaandama, Mrundi, Amis Tambwe, Mzimbabwe, Donald Ngoma na Chirwa.
Kuendelea kwake kufunga magoli kunaipa nafasi timu yake kuendelea kupanda juu kimsimamo kwani licha ya kufunga magoli sita tu katika michezo sita iliyopita ila safu ya ulinzi imekuwa imara na hata magoli matatu waliyoruhusu hadi sasa hajawaathiri sana.
Ajib ni namba 10
Uwepo wa Pius Buswita katika kikosi cha Yanga hivi sasa kumekumeongeza ufanisi wa timu katika utengenezaji wa nafasi. Buswita anaenda sana kurahisisha mpira kwa pasi zake zake fupifupi za ‘one-two’. Katika mchezo uliopita dhidi ya Kagera Sugar kocha Lwandamina aliwapanga washambuliaji wawili-Ajib na Chirwa.
Upande wa kushoto alimpanga Geofrey Mwashuiya, Buswita akawa anaibia katika wing ya kulia-huku akisogea sana katikati wakati wakishambulia ili kumpa nafasi beki namba mbili Juma Abdul kupanda kwa ajili ya kupiga krosi pasi.
Ajib alikuwa akipata uhuru wa kushuka hadi eneo la kati la kuichezesha timu kama vile ni kiungo mchezeshaji, alipiga pasi ya juu ya kupenyeza akitokea na mpira eneo la kati na mpira ule aliuchopu na ukaangukia nyuma ya walinzi wa Kagera Sugar, Juma Nyosso na patna wake Juma Shemvuli, na kitendo cha wao kugeuka wakamkuta tayari Chirwa anautazama mpira uliodondoka mbele yake huku golikipa Kaseja akisubiri nini atafanya.
Nimeandika makala kadhaa na nimekuwa nikisisitiza Lwandamina anapaswa kutumia washambuliaji wawili wa kati wakati huu ambao nyota wake wa mashambulizi wakipambana na majeraha. Na faida niliyokuwa naitaraji ndiyo ile ambayo Ajib alionyesha. Kupiga pasi za mwisho zisizotarajiwa akitokea kati mwa uwanja, na kufunga magoli muhimu.
Baada ya kumalizika kwa mchezo wa Kagera Sugar naamini sasa, Lwandamina atakuwa amemshuhudia namba kumi bora ambaye anaweza kucheza vizuri sambamba na Chirwa au Tambwe ambao wanauwezo mkubwa wa kusimama na kutengeneza nafasi wakicheza kati zaidi. Hakika Ajib tayari ameanza kujibu matarajio ya wengi ambao waliamini angeweza kuyafanya baada ya kusajiliwa kutoka Simba msimu huu.
Alicheza akimzunguka Chirwa huku akili yake akionyesha kuwa na haraka katika kufikiria, huku akifikia maamuzi ya hatari kwa kila pasi yake iliyoelekea golini kwa timu pinzani. Aligusa mpira kiufundi, huku kiwango chake cha utendaji kazi kikiwa juu. Huyu ni namba 10 sahihi aliyekuja Yanga katika wakati mwafak

Akamatwa Akisafirisha mabomu kwenye madumu ya maji,,,,

Askari walimshtukia kijana huyo baada ya kupita kwenye vituo vitatu bila kusimama huku gari hilo likielekea kwenye kambi ya majeshi ya Umoja wa Mataifa kwa spidi kali.
Polisi mjini Kabul wamesema walitumia nguvu kubwa kumsimamisha kwa kulishambulia gari lake kwa risasi.
Kijana huyo akiwa mikononi mwa wanajeshi wa UN.
Wanajeshi wa UN nchini humo wamesema kuwa mabomu hayo yalichanganywa na mbolea na kuwekwa kwenye madumu huku mengine yakiwa kwenye maboksi ya nyanya hii ni baada ya kufanyiwa ukaguzi.
Hata hivyo, mpaka sasa hakuna kundi lolote la kigaidi lilitoa tamko juu ya tukio hilo.
Kwa mujibu wa UN nchini Afghanistan mamia ya raia wanauawa kila mwezi na makundi ya kigaidi ambapo kuanzia mwezi Januari hadi Septemba watu 1,584 wameshauawa kwenye matukio mbalimbali ya mashambulizi ya kigaidi.

Zitto amkumkumbuka Mh. Filikunjombe ‘Ni majaribu makubwa kukubali kuwa haupo nasi’

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amemkumbuka marehemu Mbunge wa jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe ambae alifariki dunia baada ya helikopta aliyokuwa akiitumia kwaajili ya kampeni kupata ajali kwenye msitu wa Selous.
Mbunge Zitto amesema kuwa Filikunjombe alikuwa rafiki yake na ndugu yake hivyo bila uwepo wake ni majaribu makubwa.
Rafiki yangu, Ndugu yangu. Miaka miwili Sasa bila kuwa nawe. Ni majaribu makubwa kukubali kuwa haupo nasi. Mola akuweke mahala peponi. Naendelea kuombea familia moyo wa subira.
Ninakukumbuka Ndugu yangu Deo Haule Filikunjombe
Mhe. Deo Filikunjombe na abiria wengine walikuwa kwenye helikopta yenye namba 5Y-DKK wakitokea Dar kuelekea Ludewa.

Ndege ya AirAsia yageuka na kurudi Australia baada ya hofu ya hitilafu

Ndege ya shirika la Indonesia ya AirAsia imelazimika kugeuka na kurudi Australia baada ya marubani kujulishwa kuwa kulikuwa na tatizo la hewa katika eneo la abiria la ndege hiyo.
Ndege hiyo ya QZ535, iliyokuwa safarini kwenda kisiwa cha Bali nchini Indonesia, ilirudi Australia dakika 25 baada ya kupaa siku ya Jumapili.
Airbus A320 iliyokuwa na abiria 151 ilitua salama kwenye uwanja wa Perth, AirAsia ilisema kuwa ndege hiyo ilikumbwa na matatizo ya kiufundi, huku vyombo vya habari nchini Australia vikisema kuwa ilionekana kushuka.
Kanda ya video iliyorekodiwa na kupeperushwa na vyombo va hahari, ilionyesha vifaa vya hewa vikining'inia kutoka kwa dari la ndege.
AirAsia iliwaomba msamaha abiria kwa tatizo lolote lililosababishwa na hitilafu hiyo.
Mwezi Juni ndege ya AirAsia iliyokuwa safarini kwenda Bali, ililazimika kurudi uwanja wa Perth baada ya hitilafu ya injini yake kusababisha ndege hiyo kutingishika kama mashine ya kuosha.
Mwezi Disemba mwaka 2014 ndege ya AirAsia ilianguka baharini na kuwaua watu wote 162 waliokuwa ndani yake

Lissu Amfaliji Nyalandu,,,,

Baada ya kukaa hospitali kwa zaidi ya mwezi mmoja Lissu
akipatiwa matibabu, Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu amekiri kuona tabasamu la Mbunge huyo aliyepigwa risasi mwezi uliopita na kuwataka watanzania waendelee na maombi.
Kupitia mtandao wake wa Instagram Nyalandu amesema kwamba shauku aliyonayo Lissu ndani ya moyo wake ni kuiona siku iliyo njema pia kufurahia siku kila asubuhi.
Nyalandu ameandika "Tuendelee kumwombea ndugu yetu Tundu Lissu. Nimeliona tabasamu la uso wake leo, na hakika Mungu anaendelea kujibu maombi ya Watanzania, na wote wanaomkumbuka katika sala na dua zao katika majira na saa hii ya kujaribiwa kwake".
"Tusimame pamoja naye, kwa kuwa shauku ya moyo wake ni kuiona siku iliyo njema, aweze kuifurahia kila asubuhi kama apendavyo Mungu".
Lissu alipigwa risasi na watu wanaodaiwa kuwa wasiojulikana tangu Septemba 07 akiwa mjini Dodoma nje ya nyumba yake alipokuwa ametoka Bungeni kutekeleza majukumu yake na sasa bado yupo hospitali ya Nairobi nchini Kenya akiendelea na matibabu.

Mwanafunzi Aua wenzie 5 kwa Risasi,,,,

Wanafunzi watano na mlinzi wa shule wameuawa kwa kupigwa risasi na mwanafunzi mwenzao, huku wengine 17 wakijeruhiwa katika shule ya sekondari ya Lokichogio iliyopo kaunti ya Turkana, nchini Kenya.
Tukio hilo limetokea mwishoni mwa wiki hii ambapo mwanafunzi huyo aliyetambulika kwa jina la Abraham mwenye asili ya SUdan Kusini alikwenda shuleni akiwa na wenzake, na kuanza kuwamiminia risasi wanafunzi ambao walikuwepo kwenye shule hiyo, kwa kinachoaminika kuwa ni kulipiza kisasi baada ya kusimamishwa sule kwa utovu wa nidhamu.
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema mwanafunzi huyo alifanikiwa kuingia shuleni hapo baada ya kumuua mlinzi na kisha kuingia bwenini, na kufanya shambulio lililopelekea vifo hivyo na kujeruhi wengine.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo amesema kuna ulazima wa kukagua wanafunzi wanaotoka maeneo ya karibu kabla hawajawasajili kwenye shule zao, ili kujiepusha na matukio kama hayo kuendelea kutokea.
Mtuhumiwa huyo ambaye alikuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza alikamatwa na polisi akijaribu kukimbia kuelekea kwenye kambi ya wakimbizi ya SUdan Kusini, na kumpeleka kituo cha polisi, lakini baada ya muda wananchi walivamia kituo hiko na kukishambulia, wakitaka kumuua kwa mawe.
Kufuatia tukio hilo uongozi wa shule hiyo umetangaza kuifunga shule hiyo kwa muda, ili wanafunzi wakae sawa kisaikolojia, kufuatia kile walichokishuhudia.