Sunday, 15 October 2017

Bodi mpya ya ligi kuu kujulikana leo

Kamati ya Uongozi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), leo inatarajiwa kupata viongozi wapya kufuatia uchaguzi mkuu utakaofanyika leo Oktoba 15 kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salam.
Jumla ya wajumbe 44 wanashiriki Mkutano huo wa uchaguzi wa Baraza Kuu la TPLB. Wajumbe hao ni klabu 16 za Ligi Kuu, klabu 24 za Ligi Daraja la Kwanza na wawakilishi wanne wa klabu za Ligi Daraja la Pili.
Wanaowania nafasi ya Mwenyekiti wa TPLB ni Clement Andrew Sanga kutoka Yanga na Hamad Yahya Juma wa Mtibwa Sugar. Nafasi ya makamu mwenyekiti inawaniwa na Shani Christoms Mligo wa Azam FC.
Nafasi tatu za kuwakilisha klabu za Ligi Kuu kwenye Kamati ya Uongozi zinawaniwa na wagombea wawili ambao ni Hamisi Mshuda Madaki (Kagera Sugar) na Ramadhani Marco Mahano (Lipuli).
Almasi Jumapili Kasongo kutoka Ashanti United FC amejitokeza kuwania nafasi ya uwakilishi wa klabu za Ligi Daraja la Kwanza. Wakati Edgar William Chibura kutoka Abajalo FC anawania nafasi ya uwakilishi ya klabu za Ligi Daraja la Pili kwenye Kamati ya Uongozi ya TPLB.

Trump hana uwezo wa kufuta mkataba wa nyuklia na Iran - Mogherini

Muakilishi wa Umoja wa Ulaya wa mambo ya njee Federica Mogherini asema kuwa rais Trump hana uwezo wa kufıuta mkataba wa nyuklia uliosainiwa bain aya Marekani na Iran
Federica Mogherini akiwakilisha Umoja wa Ulaya asema kuwa msimamo wa rais wa Marekani Donald Trump kuhusu mkataba wa nyuklia uliosaini na Iran amesema kuwa rais wa Marekani hana uwezo wa kufut mkataba huo.
Mogherini aliyazungumza hayo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika mjini Brussels nchini Ubelgiji kunakopatikana ofisi za Umoja huo.
Umoja wa Ulaya umepinga msimamo wa Donald Trump kuhusu mkataba wa nyuklia.
Mogherini aliendelea kusema kuwa mkataba huo hauhusu taifa moja pekee kufuta mkataba huo.

Burudani : Nuh Mziwanda Afunguka maumivu anayoyapata,,,,,

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Nuh Mziwanda ambaye hivi karibuni ameachana na mke wake, amesema kuwa kitendo hicho kinamuumiza sana kwani anakosa muda wa kuwa na mtoto wake, na anahisi mtoto wake atakuwa bila kupata malezi yake.
Kwenye ukurasa wake wa instagram Nuh Mziwanda ameandika ujumbe akionyeshwa kuumizwa na kuwa mbali na mtoto wake huku akilelewa na watu wengine, wakati yeye baba yake yupo, lakini anashindwa kutimiza wajibu wake wa kumlea kutokana na ugomvi uliopo kati yake na mama mtoto wake ambaye wameshaachana, huku akijtahidi
"Nakumiss sana Mwanangu Anya, yani Mungu anajua jinsi gani Moyo wangu unaenda mbio nikikukumbuka au ukinijia akilini, maana najua haufurahi, najua hauhisi upendo kama uliokua unahisi kipindi upo karibu yangu, napenda ningekukuza kwenye misingi yangu, sheria zangu na kanuni zangu kama baba yako, ukweli nipo kwenye wakati mgumu sana sana kwa ajili yako wewe tu, najitatahidi kucheka ila ukweli naumia na majonzi mengi juu yako", ameandika Nuh Mziwanda.
Nuh Mziwanda ameendelea kuandika ujumbe huo akisema anamwachia Mungu kwa yote yanayotokea, huku akimlaumu mama mtoto wake kwa malezi ambayo anampa, kwani sio yale anayostahili mtoto wa umri wake kuyapata.

NEWS : Watu 10 wamefariki katika Ajari ya moto Saudi Arabia,,,,,,,

Moto umeripotiwa kuwaka katika warsha ya useremala mjini Riyadh nchini Saudi Arabia.
Kwa mujibu wa habari,moto huo umesababisha vifo vya watu 10 huku wengine watatu wakiwa wamejeruhiwa vibaya.
Sababu ya moto haijajulikana mpaka sasa.

MICHEZO: Ibrahim Ajib Azidi kumpoteza Niyonzima,,,,,,

Haruna Niyonzima na Ibrahim Ajib ni wachezaji waliozungumzwa sana wakati wa dirisha la usajili kabla ya kuanza kwa msimu huu kwa sababu ya kuhama kutoka klabu zao na kujiunga na mahasimu wa klabu walizozihama. Ajib kutoka Simba kwenda Yanga Niyonzima kutoka Yanga kwenda Simba.
Inatajwa kwamba Ajib alisajiliwa na Yanga kwa Tsh. 50 Mil pamoja na gari ndogo ya kutembelea (Toyota Brevis). Wakati huo ikielezwa Niyonzima ndiye mchezaji ghali kusajiliwa msimu huu baada ya kuvuta mtonyo unaokadiriwa kufika Tsh. 120 Mil.
Baada ya ligi kuanza Ajib ameshafunga magoli matatu na ku-assist moja katika mechi sita alizocheza huku Yanga ikiwa imefunga magoli sita kwenye ligi wakati Niyonzima bado hajafunga wala kutoa assist katika magoli 14 ambayo Simba imefunga hadi sasa, amecheza mechi nne kati ya tano.
Ibrahim Ajib
Njombe Mji 0-1 Yanga (Ajib)
Yanga 1-0 Ndanda (Ajib)
Kagera Sugar 1-2 Yanga (Ajib-assist goli la kwanza likafungwa na Chirwa, yeye akafunga la pili).
Haruna Niyonzima
Simba 7-0 Ruvu Shooting (hakufunga wala ku-assist)
Azam 0-0 Simba
Mbao 2-2 Simba (hakufunga wala kutoa assist)
Stand United 1-2 Simba (hakufunga wala ku-assist)
Ligi bado inaendelea bado kuna fursa ya kuona mambo mengi kutoka kwa mafundi hawa wawili ndani ya ligi yetu, Niyonzima anaweza akanyanyuka na kumfikia Ajib hata kumwacha lakini pia inawezekana Ajib akaendelea kumkimbiza Niyonzima kama ilivyo sasa hivi.

RB Leipzig yaiyadhibu Borussia Dortmund 3-2

Borussia Dortmund (4-3-3): Burki; Toljan (Pulisic 45), Papastathopoulos, Toprak, Zagadou; Castro, Sahin (Weigl 45), Gotze; Yarmolenko, Aubameyang, Philipp (Bartra 51)
Subs not used: Weidenfeller, Isak, Dahoud, Kagawa
Goals: Aubameyang 4, 64
Yellow Cards: burki 48; Gotze 72
Red Cards: Papastathopoulos 47
RB Leipzig (4-2-2-2): Gulacsi; Fernandes, Ilsanker, Upamecano, Halstenberg; Kampl, Keita (Demme 45); Sabitzer (Orban 86), Bruma; Poulsen, Augustin (Laimer 65)
Subs not used: Forsberg, Werner, Schmitz, Mvogo
Goals: Sabitzer 10; Poulsen 25; Augustin 49 (pen)
Yellow Cards: Fernandes 30; Ilsanker 54; Keita 15; Demme 83
Red Cards: Ilsanker 56

MAGAZETI YA LEO,,, OCTOBER 15


Saturday, 14 October 2017

Rais wa TFF kufungua mkutano wa Uchaguzi wa bodi ya ligi Kesho

RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia ndiye atafungua Mkutano wa Uchaguzi wa Kamati ya Uongozi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) utakaofanyika kesho Jumapili, Oktoba 15 mwaka huu, kuanzia Saa 2.00 asubuhi hadi Saa 7.15 mchana.
Kwa mujibu wa ratiba, Saa 2.00 asubuhi, Wajumbe na viongozi wengine watawasili Ukumbi wa mikutano wa Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, kabla ya mkutano huo kufunguliwa saa 3.00 asubuhi na Rais wa TFF, Wallace Karia atayekuwa Mgeni Rasmi.
Taarifa ya TFF imesema kwamba kutakuwa na mkutano na wanahabari saa 7.15 mchana mara baada ya mkutano wa Baraza hilo.
Jumla ya wajumbe 44 watashiriki Mkutano huo wa uchaguzi wa Baraza Kuu la TPLB. Wajumbe hao ni klabu 16 za Ligi Kuu, klabu 24 za Ligi Daraja la Kwanza na wawakilishi wanne wa klabu za Ligi Daraja la Pili.
Nafasi ya Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe wa kuwakilisha klabu za Ligi Kuu zitapigiwa kura na klabu 16 pekee za Ligi Kuu.
Wagombea saba wamepitishwa kuwania uongozi wa TPLB baada ya Kamati ya sasa kumaliza muda wote. Kamati mpya ya Uongozi itakayochaguliwa katika uchaguzi huo unaosimamiwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF utakaa madaraka kwa kipindi cha miaka minne.
Waliopitishwa kwenye kinyang’anyiro hicho baada ya orodha ya mwisho iliyotolewa Oktoba 9, mwaka huu ni Clement Andrew Sanga kutoka Yanga na Hamad Yahya Juma wa Mtibwa Sugar wanaowania uenyekiti wa TPLB.
Wengine ni Shani Christoms Mligo wa Azam FC ambaye ni mgombea pekee wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti. Nafasi tatu za kuwakilisha klabu za Ligi Kuu kwenye Kamati ya Uongozi zimevutia wagombea wawili; Hamisi Mshuda Madaki (Kagera Sugar) na Ramadhani Marco Mahano (Lipuli).
Almasi Jumapili Kasongo kutoka Ashanti United FC ni mgombea pekee aliyejitokeza kuwania nafasi ya uwakilishi wa klabu za Ligi Daraja la Kwanza. Klabu za Daraja la Kwanza zina nafasi mbili.
Klabu za Ligi Daraja la Pili zina nafasi moja kwenye Kamati ya Uongozi ya TPLB, na mgombea pekee aliyejitokeza kuwania nafasi hiyo Edgar William Chibura kutoka Abajalo FC.

Yanga yaishusha chini Simba na Azam baada ya kuifunga kagera sugar mabao 2-1,,,,,,,

Klabu ya soka ya Yanga imeendeleza ubabe mbele ya Kagera Sugar baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 kwenye mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara uliomalizika jioni hii kwenye uwanja wa Kaitaba, Bukoba.
Mabingwa hao watetezi wa ligi kuu wamefanikiwa kuchukua alama tatu mbele ya wenyeji wao kupitia mabao ya Obrey Chirwa na Ibrahim Ajibu wakati bao pekee la Kagera limefunga na Jafari Kibaya.
Yanga sasa imesogea hadi kileleni ikifikisha alama 12 baada ya michezo sita sawa na Azam FC ambayo imelazimishwa sare ya bao 1-1 na timu ya Mwadui FC kwenye mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Mwadui Complex.
Matokeo mengine kwenye mechi za leo ni sare ya 0-0 kati ya Njombe Mji na Lipuli FC, wakati Ruvu Shooting nayo imetoka sare ya 0-0 na Singida United. Ndanda FC wametoshana nguvu na Majimaji baada ya kufungana 1-1.

Michezo: Klopp amsifu lukaku,,,,,,

London, England. Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp amekiri kuwa wakati wote alikuwa anajua Romelu Lukaku atakuwa mshambuliaji bora dunia wakati timu yake ikijiandaa kumkabili nyota huyo wa Manchester United leo.
Lukaku amekuwa na mwanzo mzuri ndani ya Manchester United akiwa amefunga mabao 11 katika mechi 10 alizocheza za mashindano yote.
Klopp ambaye kikosi chake cha Liverpool kinawakaribisha vijana wa Jose Mourinho kwenye Uwanja wa Anfield, alisema alijua ubora wa Lukaku kabla ya kusajili kwa pauni 75milioni na Man United.
Akizungumza katika mkutano na wanahabari, Mjerumani huyo alisema: "Amekuwa bora zaidi, na pia bado ni kijana mdogo.
"Nafikiri hakuna shaka yoyote kuwa ni mshambuliaji bora duniani na alishakuwa hivyo tangu akiwa Everton.
"Na sasa yupo katika kikosi cha wachezaji bora wa Man United wanamsaidia kukua zaidi."
Man United inaingia katika mchezo huo ikiwa na lengo la kuweka rekodi mpya baada ya mechi nane inataka kuvuka idadi ya pointi 20 ilizowahi kupata katika msimu wa 2011/12 na 1999/00.
Lakini wakiwa na pengo kubwa katika safu yao ya kiungo kutokana na kuwakosa nyota wake majeruhi Michael Carrick, Paul Pogba na Marouane Fellaini.
Liverpool wenyewe wanabidi kujitazama upya katika safu yao ya ulinzi kutokana na kufanya makosa mengi katika mechi zilizopita.
Pia, watamkosa Sadio Mane aliyeumia akiwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Senegal wiki hii, hivyo Klopp atalazimika kujifikiria upya.

News: Mugabe Kumpa nafasi kubwa mkewe

Harare, Zimbabwe. Rais Robert Mugabe amekubali kugeuza kongamano la mwaka la Zanu PFlililopangwa kufanyika Desemba kuwa mkutano mkuu wa congress unaotarajiwa kutumika kumshusha Makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa na kumpaisha mkewe Grace kuwania urais katika chama.
Kamisaa wa Taifa wa Zanu PF Saviour Kasukuwere ndiye aliyependekeza suala la mkutano wa congress alipokuwa anawasilisha ripoti yake kwenye kamati kuu ya chama Jumatano lakini ilibainika kuwa kinara huyo wa kundi la G40 alikuwa amepata ushauri kutoka majimbo matatu tu.
"Mugabe alisema utakuwa ukiukwaji wa taratibu hivyo akaagiza kamati ya maandalizi kuhakikisha ushauri umepatikana kutoka majimbo yote. Kutakuwa na vikao vya uratibu wa majimbo kutafakari suala hilo kuanzia mwishoni mwa wiki hii.
"Mkutano mkuu wa chama umepangwa ili kufanya mabadiliko ya katiba ili kuingiza kifungu cha kuwa na makamu wa rais mwanamke au kuanzisha makamu wa tatu wa rais,” mtu wa ndani alidokeza.
"Suala la urais limekamilika lakini misuguano ya ndani kuhusu kuwania mamlaka na umri wa Mugabe vimelazimisha kutafakari na Nyanja mbalimbali. Kumbuka kuwa Grace anataka madaraka na amekuwa akiomba awe makamu wa rais sambamba na Mnangagwa".
Msemaji wa Zanu PF, Simon Khaya Moyo amekataa kuzungumzia suala hilo.
Miezi miwili iliyopita Mugabe aliwataka wajumbe wa Zanu PF kufikiria kuingiza katika katiba nafasi ya makamu wa tatu wa rais. Hii ilikuwa baada ya mkewe kumtaka kiongozi huyo mkongwe wa Zanu PF kumtangaza mrithi anayempendelea katika mkutano mkuu wa wanawake.

Sifuti Mwenge - Magufuri,,,,,,,

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amesema hatafuta Mwenge wa Uhuru katika kipindi chake cha uongozi kwasababu una faida mbalimbali kwa taifa.
Hayo ameyasema leo kwenye hotuba yake wakati akihitimisha mbio za Mwenge mwaka huu sambamba na kuazimisha miaka 18 ya kifo cha Baba wa Taifa kwenye sherehe zilizofanyika kwenye uwanja wa Amani Zanzibar.
Rais Magufuli amesema kwenye awamu yake kamwe hatafuta mbio hizo kwani zina saidia kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo nchini pamoja na kumuenzi Baba wa taifa Hayati Mwalimu Nyerere ambaye ndiye muasisi wa Mwenge wa Uhuru.
“Nafahamu kuna watu wanataka mbio za Mwenge zifutwe kwa kisingizio cha gharama lakini wanasahau kuwa Mwenge huo unasaidia kuanzishwa na kukamilika kwa Miradi ya maendeleo nchini. Nataka niwahakikishie kuwa kwenye uongozi wangu na Dkt. Shein hatutafuta Mwenge wa Uhuru”, amesema Rais Magufuli.
Aidha Rais Magufuli ameongeza kuwa mbio za Mwenge zimekuwa zikisaidia kubaini madudu mbalimbali yanayofanyika kwenye Halmashauri nchini ikiwemo Miradi hewa. Rais ameahidi kuipitia ripoti nzima ya mbio hizo na kuyafanyia kazi mapendekezo yote yaliyoainisha.

Rais Mgufuli afunguka kuhusu Kufuta Mbio za Mwenge,,,,,,

“Nafahamu kuna watu wanataka mbio za Mwenge zifutwe kwa kisingizio cha gharama lakini wanasahau kuwa Mwenge huo unasaidia kuanzishwa na kukamilika kwa Miradi ya maendeleo nchini. Nataka niwahakikishie kuwa kwenye uongozi wangu na Dkt. Shein hatutafuta Mwenge wa Uhuru”, amesema Rais Magufuli.
Hayo ameyasema leo kwenye hotuba yake wakati akihitimisha mbio za Mwenge mwaka huu sambamba na kuazimisha miaka 18 ya kifo cha Baba wa Taifa kwenye sherehe zilizofanyika kwenye uwanja wa Amani Zanzibar.
Rais Magufuli amesema kwenye awamu yake kamwe hatafuta mbio hizo kwani zina saidia kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo nchini pamoja na kumuenzi Baba wa taifa Hayati Mwalimu Nyerere ambaye ndiye muasisi wa Mwenge wa Uhuru.
Mara baada ya kukabidhi Mwenge wa uhuru kwa Rais John Magufuli, kiongozi wa mbio hizo Amour Ahmad Amour amemueleza salamu za Watanzania kuwa wamempongeza kwa jitahada anazofanya kuikomboa Tanzania kiuchumi, hata hivyo aliongeza kuwa mbio hizo hazikuridhishwa na utekelazaji wa miradi katika baadhi ya halmashauri nchini.
Hata hivyo Waziri Wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Na Wenye Ulemavu Jenista Muhagama amewataka Watanzania wote kulinda tunu ya amani ambayo imekuwa ikihamasishwa na Mwenge huo, na kwamba katika mbio hizo miradi yenye thamani ya shilingi trilioni 2.1 ilizinduliwa na kati yake miradi 151 ni ya viwanda, Aidaha ameongeza kuwa jumla ya miradi 21 yenye thamani ya shilingi bilioni 3.1 ilikataliwa kuzinduliwa na kuwekwa jiwe la msingi.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mahamoud amemueleza Rais kuwa mwenge huo ulikimbizwa katika wilaya zote 3 za mkoa huo ambazo ni sawa na kilimeta za mraba 65 na kushuhudiwa na wananchi takribani laki moja na elfu ishirini, hata hivyo aliongeza kuwa kupita kwa mwenge huo umesaidia kupambana na biashara haramu ya dawa za kulevya.
Mbio hizo zilianza 2017 April 2, 2017 katika mkoa wa Katavi na kukimbizwa katika mikoa yote 31 Tanzania bara na visiwani umezimwa kitaifa katika Mkoa wa Mjini magharibi Visiwani Zanzibari ilikiwa na kauli mbiu ya Shiriki kukuza uchumi wa Viwanda kwa maendeleo ya Nchi yetu
Mbali na Rais Magufuli maadhimisho hayo pia yalihudhuriwa na Makamu wa Rais wa pili Zanzibar Balozi Seif Iddi, Makamo wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu, Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa, Viongozi waandamizi serikalini, Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, wakuu wa mikoa, Wawakilishi wa vyama na mabalozi wa nchi wa mbalimbali.
Kwa mwaka 2018 uzinduzi wa mbio za mwenge utafanyika mkoani Geita na mbio hizo zitamalizikia mkoani Tanga. Rais Mgufuli afunguka kuhusu Kufuta Mbio za Mwenge
 