Monday, 29 January 2018

Audio | Gigy Money – Mimina | Mp3 Download

Audio | Gigy Money – Mimina | Mp3 Download

Audio | Gigy Money – Mimina | Mp3 Download

New VIDEO: Gigy Money – Mimina

New VIDEO: Gigy Money – Mimina

New VIDEO: Gigy Money – Mimina

DOWNLOAD VIDEO

Bunge kuunguruma kesho, wabunge watatu kuapishwa



Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajiwa kuanza kunguruma kesho (Jumanne) na Mkoani Dodoma kwa kuanza kuapisha Wabunge wapya watatu pamoja na kupitisha miswada miwili ya sheria ambayo ilisomwa kwa mara ya kwanza katika mkutano wa tisa.

Hayo yamewekwa wazi na taarifa rasmi iliyotolewa na ofisi za Bunge kupitia Kitengo cha Habari na Mawasiliano na kusema kuwataja wabunge hao ambao watakula kiapo cha uaminifu kuwa ni Mhe. Dkt. Damas Daniel Ndumbaro kutokea Songea Mjini, Mhe. Monko Justine Joseph wa Singida Kaskazini na kumaliziwa na Mhe. Dkt. Stephano Lemomo Kiruswa wa Longido.

Aidha, katika mkutano huo wa 10 kutakuwa na wastani wa maswali 125 ya kawaida yanayotarajiwa kuulizwa na Wabunge huku wastani wa maswali 16 ya kiwa ya papo kwa hapo kuenda kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu ambayo yanatarajiwa kuulizwa siku ya Alhamisi mnamo februari mosi.

Kwa upande mwingine, Kamati 16 za Bunge za kudumu zitawasilisha taarifa zake Bungeni hapo.

Lita 85 za Gongo zakamatwa Manyara


Jeshi la Polisi mkoani Manyara limesema limekamata mitambo ya kutengenezea pombe haramu ya gongo pamoja na lita 85 za pombe hiyo, ambayo ni kinyume na sheria za nchi.

Akizungumza na mwandishi wa www.eatv.tv Kamanda wa Polisi mkoa wa Manyara Agustino Senga, amesema vifaa hivyo pamoja na pombe imekamatwa kutokana na operesheni maalum inayoendeshwa na jeshi hilo.

“Mkoa wetu wa Manyara umeendelea na misako mbali mbali ambapo tumekamata mitambo ya gongo pamoja na gongo huko mbulu, kijiji cha hydom Manyara, walimkata mtu mmoja Moshi Bula mwenye miaka 55, akiwa na mitambo minne ya kutengenezea mitambo ya gongo, hivi sasa yupo mahabusu na taratibu zikikamilika atafikishwa mahakamani,”, amesema Kamanda Senga.

Kamanda Senga ameendelea kuelezea kwamba...Sambamba na hilo tumekamata lita 65 za pombe haramu ya moshi pamoja na watu watatu wanaohusika na pombe hiyo, ambao ni Neema Doto Matayo, mwenye miaka 21, Lawawa Sakara na Patrima Bula na wote watafikishwa mahakani”.

Licha ya hayo Kamanda wa Senga amesema pia wamemkatama mwanamke mmoja akiwa na lita 20 za gongo, na kufanya idadi ya lita 85 za pombe hiyo haramu.

Tani 3.5 za meno ya Kiboko zapata mnunuzi



Kampuni ya Ontour Tanzania Limited imenunua kwa Sh30.9 milioni meno ya viboko tani 3.5 yaliyokuwa yakipigwa mnada na Serikali baada ya kukusanywa kwa miaka 14.

Mnada huo umefanyika leo Januari 29, mwaka 2018 jijini Dar es Salaam na kuongozwa na kamati maalumu ya mnada inayoundwa na maofisa wa Wizara ya Fedha na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (Tawa), kuongozwa na Karerema Kwareh kutoka wizara hiyo.

Awali, Kwareh alieleza masharti ya mnada huo, huku sharti namba tano linalimtaka mnunuzi kununua mzigo wote likiibua mjadala kwa baadhi ya wanunuzi wakitaka liondolewe.

Licha ya kupingwa na wanunuzi, Kwareh amesema wazo hilo limechukuliwa na litafanyiwa kazi katika mnada ujao, si mnada wa leo.

Mfanyabiashara wa kwanza alitaka kununua meno hayo kwa Sh25.2 milioni lakini alizidiwa kete na mkurugenzi wa Ontour, Crey Kilasi aliyetoa Sh30.9 milioni.

Kaimu Mkurugenzi wa Tawa,  Mabula Misungwi amesema meno hayo yameuzwa ili thamani yake isiendelee kushuka na hatua hiyo haiwezi kuwa chachu ya kuongezeka kwa ujangili.

"Nyara hizi huwa zina thamani yake na zinavyozidi kukaa huwa thamani inashuka. Meno haya ni yale yanayopatikana kutokana na vifo vya kawaida vya viboko na yale yanayokamatwa kwa majangili," amesema Misungwi.

Amesema meno ya kiboko yana soko kubwa ulaya ambako hutumika kutengenezea urembo na bidhaa nyingine za mapambo.

Akizungumza baada ya kufanikiwa kununua meno hayo, Kilasi amesema atatumia wastani wa miezi sita kutafuta soko.

"Soko lake kubwa ni Japan na China ambapo huyatumia kama mbadala wa meno ya tembo, bei yake inaweza ikafikia Dola 25 za Marekani," amesema Kilasi.

Amesema asilimia 60 ya meno hayo ndio inaweza kuuzika vyema sokoni, huku asilimia 40 yakiwa hayapo katika hali nzuri.

VIDEO: Mbowe - Asema Mtulia Ni Gunia La Misumari

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA leo kimeendelea na kampeni zake za ubunge wa jimbo la Kinondoni ambapo Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Freeman Mbowe aliwahutubia wanachama na wafuasi wao huku akimnadi mgombea wao, Salumu Mwalimu.

"Fursa aliyoitoa Mwenyezi mungu ya kuwapa nafasi ya kuchagua mbunge makini ambae atawatetea,  inapaswa muitumie vizuri kuliko kuwa na Mbunge mzigo ambae ni gunia la misumali'' amesema Mbowe

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KU SUBSCRIBE

Waziri Jaffo atoa agizo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, Selemani Jafo amewaagiza wakuu wa wilaya na wakurugenzi watendaji wa halmashauri (DED) kutunza siri za Serikali.

Jafo ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Januari 29,2018 mjini Dodoma alipofungua mafunzo ya uongozi kwa wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa mikoa sita.

Mafunzo hayo ni mwendelezo wa ambayo yanatolewa kwa viongozi wa kada hiyo.

Waziri Jafo amesema ujenzi wa Serikali utakuwa mzuri iwapo viongozi hao watakuwa makini na kutunza siri.

"Hivi unakuwaje wewe mkurugenzi au mkuu wa wilaya unapeleka siri za Serikali kwenye mitandao ya kijamii na nyingi unaziona kwenye WhatsApp, inatia aibu sana," amesema Jafo.

Amewataka wakurugenzi kujipambanua na kusimamia miradi ya maendeleo katika kukusanya mapato na kuyatumia vyema na hasa ya ndani.

Jafo amesema tatizo kubwa kwa wakurugenzi ni kutofanya uamuzi kwa haraka.


Ndoa zilizofungishwa bila leseni kubatilishwa


Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini nchini RITA, imesema, ndoa zote zilizofungwa bila kuzingatia sheria ya ndoa ikiwemo viongozi wa dini waliofungisha ndoa hizo kutokuwa na Leseni ya kufungisha ndoa huenda zikabatilishwa.

Afisa Usajili Msaidizi wa RITA Jane Barongo, amefafanua kuwa ndoa hizo zitabatilishwa tu endapo itabainika viongozi waliofungisha ndoa hizo hawakuwa na Leseni ya kufungisha ndoa kutoka serikalini.

Barongo ameongeza kuwa kiongozi wa dini atakayebainika kufungisha ndoa bila kuwa na Leseni ya serikali anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria ya ndoa ambayo imeipa Rita mamlaka ya kisheria, kusajili ndoa zote zilizofungwa kihalali.

Kwa upande mwingine amesema tayari serikali imewakumbusha viongozi wote wa dini kuhakikisha wanakamilisha taratibu za kukata Leseni ya kufungisha ndoa kabla ya kufungisha ndoa yoyote nchini.

Ang'oa paa la nyumba anayoishi mke wake


Mwanaume mmoja aliyejulikana kwa jina la David Kinyua mkazi wa Gichiche nchini Kenya ameng'oa mabati ya nyumba anayoishi mke wake ambaye anadai amempangisha, akimtuhumu amekaa muda mrefu ndani ya nyumba hiyo kinyume na makubaliano.

Kwenye tukio hilo ambalo limeleta sintofahamu kwa majirani, limeelezwa kwamba Bwana Kinyua ambaye ni mume wa Juliet Karimi alifanya tukio hilo, ili mke wake huyo aweze kuhama na kupisha mpangaji mpya.

“Nilipanga kukarabati nyumba baada ya Julieti kutoka, ili mpangaji akija akute nyumba yenye hali ya kupendeza, lakini amekataa kutoka, na alisaini makubaliano kama mpangaji kufuata utaratibu”, amesema bwana Kinyua.

Upande wa mke wake Bi. Juliet Karimi ambaye ndiye mke alikutwa na balaa hilo, amesema ameshangaa kuona watu wamekuja kutoa paa la nyumba kwenye nyumba anayoishi, na hata haelewi ni kwa namna gani aliishia kuwa mpangaji kwenye nyumba aliyoshiriki kujenga.

'Nilichangia kiuchumi kwenye kujenga nyumba hii, nashangaa haya yanatokea, naomba wanaohusika na masuala ya sheria inisaidie nipate haki yangu”, amesema Julieth ambaye amepangishwa kwenye nyumba aliyoshiriki kujenga yenye vyumba vinne.

Majirani wa wawili hao wamesema wanamfahamu Juliet kama mke wa David, na sio mpangaji kama anavyodaiwa.


Mourinho aweka rekodi nyingine Man Utd


Kocha wa Manchester United Jose Mourinho ametimiza mechi 100 tangu ajiunge na timu huku akiwa na wastani mzuri wa ushindi akiwazidi makocha waliomtangulia akiwemo Sir Alex Ferguson.

Mourinho ambaye alijiunga na United majira ya kiangazi mwaka 2016 amedumu na klabu hiyo kwa msimu mmoja na nusu sasa, na hivi karibuni ameongeza mwaka mmoja kwenye mkataba wake uliokuwa unamalizika 2019.

Katika mechi zake 100 Mourinho amefanikiwa kuiongoza United katika mechi za EPL 62 ambapo ameshinda 34, sare 20 na kufungwa 8. Katika mechi 6 za UEFA Mourinho ameshinda 5 na kupoteza moja.

Kwa upande wa EUROPA Mreno huyo ameshinda mechi 10 akitoka sare mara tatu na kupoteza mbili. Kwa upande wa Kombe la FA amecheza mechi 6 akishinda 5 na kupoteza moja. Kombe la Ligi EFL kocha huyo ameshinda mechi saba na kupoteza mbili.

Kwa upande wa makocha waliomtangulia Ferguson alishinda mechi 48, Moyes ambaye alikomea mechi 51 alishinda 27 pekee huku Louis Van Gaal akishinda mechi 52. Mourinho yupo juu yao akiwa ameshinda jumla ya mechi 62.


Mwijage atoa rai kwa uongozi wa Chuo cha CBE




Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage ameutaka uongozi wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kutoa elimu ya ujasiriamali ili wahitimu waweze kujiajiri.

Akizindua bodi ya CBE jana, Mwijage alisema ujasiriamali liwe somo la lazima ili kukabiliana na tatizo la ukosefu wa ajira.

“Katika zama hizi na tunakokwenda, kuajiriwa itakuwa zilipendwa, hivyo tuwafundishe vijana ili wawe na uwezo wa kuajiriwa na kujiajiri,” alisema Mwijage.

Alifafanua kuwa zamani wahitimu wa vyuo vikuu walitegemea ajira za Serikali lakini sasa hali iko tofauti.

Mwijage alisema chuo hicho kinatakiwa kutoa elimu itakayowasaidia kuwa na mbinu nyingi za ubunifu na kujiajiri.

Mwenyekiti mpya wa bodi, Ester Ishengoma alimhakikishia waziri kuwa bodi hiyo inafuata maelekezo yake kwa lengo la kukiboresha chuo hicho.

Kumbe Ngassa bado anaidai Mbeya City



Kiungo mshambuliaji wa Ndanda FC, Mrisho Ngassa, amesema kuwa amechoka usumbufu wa kuidai klabu yake ya zamani, Mbeya City, mshahara wake wa miezi minne, lakini akasisitiza anaomba fedha zake.

Ngassa alijiunga na Ndanda hivi karibuni katika usajili wa dirisha dogo akitokea Mbeya mara baada ya mkataba wake kumalizika kabla ya kugoma kumuongezea mwingine.

Ngassa alisema kuwa anaidai klabu hiyo shilingi milioni 4.8 alizotakiwa alipwe tangu Desemba, mwaka jana.

Ngassa alisema amefikia hatua ya kuweka wazi madai hayo baada ya hivi karibuni viongozi wa timu hiyo kumwambia watampatia fedha hizo baada ya kulipwa fedha kutoka Azam TV ambao wanadhamini klabu za ligi kuu.

“Nimechoka kuongopewa na viongozi wa Mbeya City, kwani kila wakati nikiwapigia simu kudai malipo yangu ya mshahara ambayo ni shilingi milioni 4.8 wamekuwa hawapokei simu.

“Lakini hata wakipokea wakati mwingine wananipiga Kiswahili, kwa maana ya kunitajia siku nyingine na hivi karibuni walinipa maneno mazuri ya kuwa watanilipa fedha zangu baada ya wao kulipwa na Azam TV.

“Ninajua tayari wamepatiwa fedha hizo, lakini wamejikausha kunilipa fedha hizo ambazo ninadai hadi leo (jana Jumapili), hivyo nimechoshwa nao, naomba wanilipe fedha zangu,” alisema Ngassa aliyewahi kuzichezea Simba, Yanga na Azam FC.


Alipotafutwa jana mchana, Katibu Mkuu wa Mbeya City, Emmanuel Kimbe, alisema hayupo katika nafasi nzuri kuzungumzia suala hilo.

Kampeni za Kinondoni CHADEMA, CCM wazidi kutifuana


Wagombea ubunge jimbo la Kinondoni, Maulid Mtulia (CCM) na Salum Mwalimu (Chadema) wameendelea kujinadi katika mikutano ya kampeni, huku Mtulia akiwashangaa wanaobeza kujiondoa kwake CUF na kujiunga na chama tawala.

Wakati Mtulia akimwaga sera leo Jumatatu Januari 29, 2018 katika uwanja wa Hananasif Kinondoni, Mwalimu alikuwa uwanja wa Mtambani kata ya Mzimuni.

Tangu kuanza kwa kampeni hizo, hoja ya hamahama ya madiwani na wabunge imekuwa ikitawala kutokana na CCM kujikita kuzungumzia sababu za mgombea wake wa Kinondoni, Mtulia kuteuliwa kuwania tena nafasi hiyo, huku Chadema wakitumia kete hiyo kumnadi Mwalimu.

 “Nyalandu (Lazaro-aliyekuwa mbunge Singida Kaskazini) na Godwin Mollel (Siha) nao walihama vyama vyao lakini mimi ndiye nazungumzwa sana na kusema kila chama kimepoteza mbunge wake lakini kuna chama kimeumia kuliko vingine,” amesema na Mtulia.

Amesema, “Wakati nikiwa upinzani sikuwa na namba ya Rais, sasa ninayo mkiwa na matatizo mnaniambia mimi nampigia na mambo yanatekelezwa. Kama kawaida yake yuko kwa ajili ya kuwaletea maendeleo wananchi wote bila ubaguzi.”

Kama ilivyo kwa Mtulia, Dk Mollel naye alikuwa mbunge wa Chadema jimbo la Siha lakini Desemba 14,2017 alihamia CCM na kupitishwa kuwania ubunge huku Nyalandu ambaye alikuwa mbunge kwa tiketi ya CCM, alihamia Chadema.

Akizungumza katika kampeni hizo Mtulia amesema, “Nitakuwa mbunge wa chama dola na ninakwenda kutekeleza ilani ya uchaguzi, mtu yeyote asijaribu kuzuia ilani hii kutekelezwa. Naomba kila mmoja awe mwakilishi wangu wa kuniombea kura. Ukichagua Mtulia umechagua maendeleo.”

Akiomba kura, Mwalimu alisema, “Naahidi kwenda kuwa mbunge wa kuwatumikia wananchi wote si Chadema tu. Siendi kuwa mbunge mnafiki, nitatumia talanta zote na ninaahidi makazi bora Kinondoni, kuna changamoto ya mafuriko.”

Mwalimu amesema, “Naahidi  tutatenga fedha kuondoa mafuriko. Kuna tatizo kubwa la afya, tuna kata nne tu zenye zahanati na kituo kimoja cha afya. Napaswa kusimamia afya. Naenda kusimamia, hakuna bodaboda wala mama ntilie atakayenyanyaswa.”