Saturday, 27 January 2018

VIDEO: Full Video CCM Wakizindua Kampeni Kinondoni


Chama cha Mapinduzi CCM kimezindua kampeni zake za Ubunge wa jimbo la Kinondoni huku Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba pamoja na Waziri wa zamani wa Maji, Steven Wassira wakimnadi mgombea wa Chama hicho, Maulid Mtulia.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI...USISAHAU KUSUBSCRIBE

Kauli ya Jaji Mkuu yaamsha upya hoja ya mgawanyo wa madaraka


Kauli ya hivi karibuni Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma kuwa viongozi wa Serikali na wanasiasa wasiingilie Mahakama na kudharau amri za mhimili huo, imeamsha upya hoja la mgawanyo wa madaraka baina ya mihimili mitatu ya dola ambayo imekuwa mjadala kwa muda mrefu.

Mjadala kuhusu mgawanyo huo wa Serikali, Bunge na Mahakama umekuwapo nchini kwa muda mrefu hasa wakati wa mchakato wa mabadiliko ya Katiba kuwa inaonekana Serikali ama inaizidi nguvu au inaingilia shughuli za mihimili mingine, licha ya kwamba yote hiyo inatakiwa kuonekana sawa.

Hata hivyo, baadhi ya watu huamini kwamba mhimili wa Serikali ambao unaongoza dolo ndio wenye nguvu kwa kuwa unasimamia mapato na matumizi ya mihimili mingine.

Hata Rais John Magufuli alipozungumza na wahariri wa vyombo vya habari kuhusu suala hilo Novemba 2016, alisema, “Mihimili hiyo (Bunge, Serikali na Mahakama) inaweza ikalingana, lakini inawezekana kuna mhimili ambao umechimbiwa zaidi kwenda chini.”

Akisisitiza jibu lake, Rais alizungumzia jinsi alivyokwenda kwenye shughuli ya mahakama na akaombwa fedha na uongozi wa mhimili huo kwa ajili ya uendeshaji wa shughuli zake kwa kutambua kuwa, Rais ndiye mwenye uwezo wa kuwapatia fedha hizo.

Ndani ya mjadala huo, pia yamekuwapo madai miongoni mwa wananchi kupitia maoni yao wakati wa mchakato wa Katiba, wanasiasa, wanaharakati kuwa Serikali imekuwa inaingilia shughuli na mihimili mingine – Bunge na Mahakama, jambo ambalo linaathiri uhuru wake.

Pengine ni kutokana na madai hayo au mengine, ndipo Jaji Mkuu anaibuka na ujumbe mahususi kuhusu maandalizi ya maadhimisho ya Wiki ya Sheria kwa Serikali;

“Nawasihi viongozi wote wa Serikali wenye mamlaka za kikatiba na kisheria, wabaki ndani ya maeneo yao ya kikatiba na wajiepushe na kuingilia maeneo yaliyo ndani ya haki, hadhi na mamlaka ya Kikatiba ya Mahakama.”

Akaongeza kwamba kuanzia sasa (Mahakama) watakuwa wakali kwa mtu atakayeingia katika anga zao, huku akiwataka mahakimu na majaji kuchukua hatua kwa watu wanaodharau amri zao, kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, mamlaka ya utoaji haki ni ya Mahakama pekee.

Hata hivyo, akijibu kwa nini aliamua kutoa kauli hiyo, Jaji Mkuu anasema ni kutokana na taarifa za vyombo vya habari ambavyo vimekuwa vikiripoti matukio hayo ya amri za Mahakama kuvunjwa.

Hakuishia hapo, Jaji Mkuu akawataka mahakimu ambao kwa bahati mbaya amri zao zinavunjwa na wanaonekana hawachukui hatua waanze kufanya hivyo kama Bunge linavyofanya, kwamba ukiingia katika anga zake, utaitwa mbele ya kamati, utaulizwa maswali na hatua zinachukuliwa.

Jaji Mkuu anasema Mahakama ina nguvu kama hiyo na si Jaji Mkuu mwenye nguvu hiyo pekee bali kwenye kila Mahakama; mahakama za mwanzo, mahakama za wilaya na mahakama za hakimu mkazi na asitokee mtu akajivika kofia ya kimahakama, atachukuliwa hatua.

Jaji Juma anasema kwa mujibu wa Katiba, sheria ndio inayotakiwa ipewe nguvu na si masuala ya kisiasa kwa kuwa nguvu ya Serikali ni sheria na si mtu.

“Sheria ikikupa nguvu unaitumia, ikikupa mamlaka unayatumia. Siasa haikupi nguvu, sheria ndio inakupa nguvu na tujaribu tubaki ndani ya sheria na ndani ya Katiba hakutakuwa na mvurugano. Vilevile tunawataka wale ambao wamepewa mamlaka yao, wabaki huko waliko na tukifanya hivyo hatutakuwa na migongano yoyote,” anahitimisha.

Kauli hiyo ya inaungwa mkono na Ibara ya 107 A (1) ya Katiba ya Tanzania inayosema: “Mamlaka ya utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano itakuwa mikononi mwa Mahakama ya Tanzania na Mahakama ya Zanzibar, na kwa hiyo hakuna chombo cha Serikali wala cha Bunge au Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kitakachokuwa na kauli ya mwisho katika utoaji haki.”

Mjadala mtandaoni

Muda mfupi baada ya maelezo hayo, Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter, “Mh Jaji Mkuu kauli kuhusu wanasiasa na watendaji wa Serikali kutokuingilia Mahakama ni kauli muhimu kwa wakati huu, lakini Mahakama ambayo ni imara katika haki inawezaje kukubali kuingiliwa? Mahakama inapaswa kujitazama zaidi. Mahakama ikiyumba Taifa linayumba.”

Si Lema tu aliyezungumzia hilo, wananchi wengine mbalimbali walitoa maoni yao kuhusu kauli hiyo kupitia ukurasa wa Facebook wa Mwananchi, Twitter na Instagram, huku wengine wakienda mbali zaidi kwa kumtaka Jaji Mkuu kuwaeleza maneno hayo wafuasi wa CCM, wakidai kwamba wapinzani hawana jeuri ya kuingilia Mahakama.

Kwa jinsi mjadala ulivyokwenda ni wazi kuwa Jaji Mkuu Profesa Juma ameona kuna kitu ambacho pia wananchi wanakiona hakiendi sawa na kuamua kufikisha ujumbe wake kwa njia hiyo.

Wachambuzi wa masuala ya siasa wanatafsiri kauli ya Jaji Mkuu kama “kuchoshwa kwa mhimili huo kuingiliwa na hivyo ameamua kufikisha ujumbe kwa wenye tabia hizo ili waache mara moja.

Hatua ya Jaji Juma bila shaka ni ya kupongezwa kwani si tu imeonyesha kwamba mahakama imezinduka na kutambua wajibu na nguvu zake na hivyo inafungua pazia la demokrasia na mgawanyo wa madaraka baina ya mihimili hii mitatu ya dola.

Hatua hiyo ikizingatiwa na kutekelezwa itasaidia kuifanya mahakama iaminike na kiwe chombo pekee kimbilio kwa kila mtu kwa ajili ya utoaji haki.

Ingawa Jaji Mkuu hakutoa mifano ya matukio ya kuingilia uhuru wa mahakama, mifano ipo mingi, mfano wameshuhudiwa baadhi ya watendaji wa Serikali wakiamuru ubomoaji wa nyumba ambazo inadaiwa zimejengwa katika hifadhi ya barabara, zikiwamo zilizokuwa na amri ya mahakama ya kuzuia zisibomolewe.

Mbali na mahakama, hivi karibuni Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe aliwakaririwa akisema hata Bunge limekuwa likifanya kazi kwa kuingiliwa na Serikali.

“Maneno na vitendo vya Rais vinaashiria kuwa Bunge halina uhuru wake na mimi kama mbunge nina wajibu wa kuonyesha kutopendezwa kwangu,” alisema Zitto kupitia mtandao wa Twitter na kuongeza kuwa “Ni dalili ya wazi ya kufifisha sauti ya Bunge na kupandisha sauti ya Serikali.

Moja ya matukio ambayo mbunge huyo alitaja kama kuingilia mhimili huo ni kuzuia matangazo ya moja kwa moja ya Bunge kwa kigezo cha gharama, huku hata vituo binafsi ambavyo vilipanga kurusha Bunge moja kwa moja bila malipo vikizuiwa.

Akijadili suala la uhuru wa mahakama na kauli ya Jaji Mkuu, Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Onesmo Olengurumwa anasema kwa muda mrefu wanasiasa na watetezi wa haki wamekuwa wakipigia kelele suala hilo lakini halikuonekana kufanyiwa kazi, hivyo hatua ya Jaji Mkuu italeta matumaini yalikuwa yametoweka.

Anasema katika suala la utoaji haki, Mahakama inapaswa kusimama kwa miguu yake isishurutishwe na isiingiliwe; majaji wazingatie sheria wakati wa kutoa hukumu.

Haiingii akilini kwamba mahakama inatoa amri fulani, lakini watendaji walioko chini ya Serikali wakapuuza na wakaendelea na shughuli zao kana kwamba hakuna amri yoyote,” anasisitiza.

“Jaji Mkuu yuko sahihi kama kweli anamaanisha. Kwa muda mrefu tumeshuhudia viongozi mbalimbali wakiwamo wakuu wa wilaya wakijitokeza kuingilia mhimili huo na kusababisha ama kupingana au kuwagawa na matokeo yake wanashurutishana na kutishana hadharani.”

Onesmo anasema hata kama Mahakama imekosea, kuna utaratibu wa kisheria wa kufuata ili kuipinga na si kama hali ilivyo sasa.

Anasema kuwa jambo hilo la kuingiliwa Mahakama likiachiwa liendelee litasababisha athari kuu tatu kwa jamii na kuzitaja kuwa ni pamoja na kuvunja Katiba.

Mosi, anasema mahakama ni chombo cha kutoa haki na endapo haitakuwa huru, ni wazi kuwa Katiba itakuwa inavunjwa na mwananchi atakosa haki zake za msingi.

Pili, anasema tatizo jingine ni kutengeneza Taifa lisilo fuata utawala wa kisheria na kwamba watu wataamua wanavyotaka wao, jambo ambalo litakuwa si zuri kwa mustakabali wa nchi.

“Jingine, ni kuingia katika migogoro isiyo na tija; itafika wakati wananchi watachoshwa na matendo hayo na kusababisha migogoro mikubwa na matokeo yake hayatakuwa mazuri,” anasisitiza Mratibu huyo wa masuala ya haki za binadamu.

Ni kutokana na umuhimu huo na mjadala mpana katika mchakato wa Katiba ikawekwa ibara ya 169 inazungumzia kwa kina uhuru wa mahakama.

Katiba inayopendekezwa

196 (1) Katika kutekeleza mamlaka ya utoaji haki, Mahakama zote zitaongozwa na masharti ya Katiba hii na hazitaingiliwa ama kwa kudhibitiwa, kushinikizwa au kupewa maelekezo na mtu au chombo chochote.

(2) Nafasi ya madaraka ya Jaji wa Mahakama ya Juu, Mahakama ya Rufani au Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano haitafutwa wakati wowote ule ikiwa kuna mtu ambaye kwa wakati huo anashikilia nafasi hiyo.

(3) Mishahara na malipo mengine ya Majaji wa Mahakama ya Juu, Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano yatalipwa kutoka katika Mfuko Mkuu wa Hazina.

(4) Mshahara na malipo mengine yanayolipwa kwa Jaji wa Mahakama ya Juu, Mahakama ya Rufani au Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano hayatabadilishwa kwa maana ya kumuondolea faida Jaji husika.

(5) Malipo ya mafao ya kustaafu ya Jaji wa Mahakama ya Juu, Mahakama ya Rufani au Mahakamu Kuu ya Jamhuri ya Muungano hayatabadilishwa kwa maana ya kumuondolea faida Jaji husika wakati wote wa uhai wake.

(6) Jaji wa Mahakama ya Juu, Mahakama ya Rufani, Mahakamu Kuu ya Jamhuri ya Muungano au Mahakama Kuu ya Zanzibar hatashtakiwa kwa jambo lolote alilolifanya au kutolifanya kwa nia njema katika   

Mwananchi. 

Chadema yazidi kukimbiwa na madiwani wake



Wimbi la madiwani wa Chadema kujivua uanachama na kujiunga na CCM limezidi kukikumba chama hicho kikuu cha upinzani nchini baada ya leo Januari 27, mwaka 2018 madiwani wake wanne kujiunga na chama tawala, wakiwemo watatu wa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo  mkoa wa Kilimanjaro.

Wakati diwani wa Kimara (Chadema), Pachal Manota akitambulishwa katika uzinduzi wa kampeni za ubunge za chama hicho jimbo la Kinondoni zilizofanyika viwanja wa Biafra, wenzake watatu walitambulishwa kwenye mkutano wa kampeni za ubunge jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro uliofanyika eneo la Makiwaru.

Madiwani hao ni Juliana Malamsha, Martha Ushaki (wote Viti maalum) na Frank Umega (kata ya Kelamfua).

Wametambulishwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo wakati akimnadi mgombea ubunge wa chama hicho jimbo la Siha, Dk Godwin Mollel.

Mpogolo amesema viongozi wa upinzani wanajiunga na CCM baada ya kubaini ajenda ya kuwahudumia wananchi, kuwaletea maendeleo ipo katika chama tawala pekee .

"Kuna  wimbi kubwa la viongozi wa upinzani kujiunga na CCM. Hii inatokana na viongozi hao kubaini kuwa ajenda ya huduma na maendeleo iko katika chama hiki pekee. Tupeni Dk Mollel ili tuweze kutekeleza agenda hii muhimu,” amesema Mpogolo.

Uamuzi wa madiwani wa Chadema kuhamia CCM mpaka sasa umeziweka Halmashauri tano zilizo chini ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kuwa hatarini kuchukuliwa na CCM.

Halmashauri hizo ni Arusha, Arumeru, Hai, Siha na Iringa ambazo madiwani wake, hasa kutoka Chadema wametimkia CCM kutokana na sababu tofauti, kubwa ikiwa ni kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais John Magufuli.

Ahadi ya Jafo Siha yafananishwa na rushwa


Wasomi wameifananisha na rushwa ya uchaguzi ahadi iliyotolewa kwa wananchi wa Jimbo la Siha kuwa watapata neema iwapo watamchagua mgombea wa CCM, Dk Godwin Mollel ambaye anatetea ubunge aliouachia mwishoni mwa mwaka jana kwa kujivua uanachama wa Chadema.

Ahadi hiyo ilitolewa juzi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Selemani Jafo wakati akimnadi mgombea Dk Mollel.

Wamesema kauli hiyo inaweza kusababisha ushindi wa Dk Mollel kupingwa, huku Profesa Abdallah Safari akienda mbali zaidi na kufananisha kauli hiyo na iliyowahi kutolewa na mawaziri kadhaa wakati wa uchaguzi mdogo wa ubunge Igunga mwaka 2011 na kusababisha ushindi wa aliyekuwa mgombea wa CCM, Dk Dalali Kafumu kubatilishwa na Mahakama.

Akiwa jukwaani, Jafo alisema CCM ndicho chama chenye Serikali na ndicho kinachoweza kutatua changamoto na shida za wananchi, na kwamba akishinda Serikali itafanya kila njia kuboresha maisha ya wananchi.

Jafo alisema ikiwa wananchi watamchagua Dk Mollel ambaye hivi karibuni alijiondoa Chadema na kugombea tena nafasi hiyo kupitia chama tawala, Serikali itashirikiana naye na miaka miwili iliyobaki Siha itakuwa moja ya wilaya ambazo zitapiga hatua kubwa na kufanya vizuri katika utekelezaji wa maendeleo.

Lakini ahadi hiyo ya Waziri Jafo kwa wananchi wa Siha haijapokelewa vizuri na wasomi waliohojiwa na Mwananchi.

“It is a sort of (ni kama-rushwa) kwa wapiga kura kupitia miradi ya maendeleo ya Serikali, anaposema Dk Mollel akishinda ndipo hospitali ijengwe,” alisema Dk Hamad Salim, mhadhiri wa sayansi ya siasa wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Dk Salim alisema kauli hiyo inaashiria rushwa na kushauri mawaziri watenganishwe na vyama vya siasa.

“Kuna haja ya kutenganisha mawaziri na vyama vya siasa. Mawaziri wanapaswa kuwa watendaji wa Serikali. Kauli ile inakera mno. Ni afadhali tu angesalimia na kuongea kama mwana CCM kuliko kuihusisha Serikali,” alisema.

Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Richard Mbunda alisema kauli ya Jafo inakwenda kinyume na sheria ya gharama za uchaguzi.

“Sheria ya gharama za uchaguzi iliyoanzishwa mwaka 2010 haikusikika sana kwenye uchaguzi wa 2015, lakini inaeleza vizuri. Kifungu cha 21(a) na (c) vinakatza hata mgombea tu kuahidi kutoa zawadi ili achaguliwe, kwa sababu itahesabika kama rushwa?” alisema Dk Mbunda.

Naye Profesa Safari alisema ikiwa mgombea wa Chadema katika jimbo hilo, Elvis Mosi atashindwa katika uchaguzi huo, wataitumia kauli ya Jafo kupinga matokeo mahakamani.

Katika ufafanuzi wake, Profesa Safari alisema kauli ya Jafo inaashiria utoaji wa rushwa na inaweza kusabababisha kesi kama ya Jimbo la Igunga.

“Hiyo ni corruption (rushwa) kabisa na ndiyo maana ile kesi ya Igunga tulishinda,” alisema Profesa Safari ambaye ni makamu mwenyekiti wa Chadema-Bara.

“Ni kauli mbaya sana na inaweka mazingira ya kupinga uchaguzi huo endapo mgombea wa CCM atashinda. Kesi ya Igunga imekuwa ikirejewa katika kesi nyingi tu.”

Hata hivyo, mkurugenzi wa taasisi ya Fordia, Buberwa Kaiza amesema kauli ya Jafo inaweza isihesabike kama rushwa kwa sababu hospitali yenyewe haijajengwa, japo kimaadili kutoa ahadi kama hiyo ni kosa.

“Maadili ya uchaguzi yanazuia kabisa mtu kutumia mali za Serikali kufanyia kampeni chama cha siasa. Maadili pia yanazuia kabla na baada ya uchaguzi kutumia majukumu ya Serikali kama ahadi ya uchaguzi,” alisema.

“Kama ilani ya uchaguzi ya CCM ilisema watajenga hospitali na yeye alikuwa akikumbushia, sawa. Lakini kama alisema mgombea wao akichaguliwa ndipo watajenga, hilo ni kosa.”

Wakimbizi kutoka Kongo wazidi kumiminika nchini


Zaidi ya raia 800 kutoka jamhuri ya kidemikrasi ya Kongo wamewasili mjini kigoma kuomba hifadhi ya ukimbizi nchini wakidai kukimbia vita katika nchi hiyo.

Raia hao wa DRC ambao wengi ni wanawake na watoto wametokea mashariki ya nchi hiyo na wamewasili kwa maboti kwa nyakati tofauti katika bandari ndogo ya Kibirizi mjini kigoma na kueleza kuwa hali ya vita katika nchi hiyo ni mbaya na kuomba serikali ya Tanzania kuwapokea.

Mkuu wa mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga akiambatana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa amefika katika eneo hilo na kueleza kuwa wamewapokea lakini serikali inafanya tathmini ya ujio wao.

Ujenzi wa reli ya kisasa watarajiwa kuanza Machi mwaka huu


Serikali imesema ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) kutoka Morogoro hadi Makutopora mkoani hapa ambao utaanza kabla ya Machi mwaka huu, utagharimu dola 1.923bilioni za kimarekani (sawa na Sh4.3 trilioni).

Meneja Mradi huo wa Kampuni Hodhi ya Raslimali za Reli (Rahco) Mhandisi Maizo Mgedzi amesema mradi huo unatarajia kuanza wakati wowote kabla ya Machi.

Amesema  treni hiyo ina uwezo wa kwenda kilometa 160 kwa saa itahifadhi mazingira na kwamba itaweza kubeba mzigo mkubwa kwa zaidi ya mara tano ya reli ya sasa.

“Pia itaweza kubeba watu na mizigo kwa usalama kwa maana  hakutakuwa na ajali zinazosababishwa na ubovu wa miundombinu,” amesema

Meneja wa Kampuni ya Yapi Merkezi iliyopewa zabuni ya mradi huo, Abdullah Kilic amesema kuwa jiwe la msingi la mradi huo litawekwa wakati wowote kuanzia sasa.

“Tunachosubiri ni utaratibu wa Ikulu lakini jiwe la msingi tutaliweka wakati wowote kuanzia sasa,”amesema.

Mbunge wa jimbo la Dodoma Mjini, Antony Mavunde amesema Serikali ingependa mradi huo ulete matokeo chanya kwa watu wa Dodoma na si laana.

“Matokeo haya yasiwe laana kwa maana tusije kuiacha reli hii ipite tu hapana. Sisi tunataka kwa watu wa Dodoma reli hii iwe kichocheo cha kwanza cha uchumi ikiwezekana kubadilisha mji,”amesema.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kongwa alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Deogratius Ndejembi amesema viongozi watawapa ushirikiano wa kutosha katika kipindi cha miaka mitatu cha ujenzi wa reli hiyo na kurekebishana kwa baadhi ya mambo.

“Wamesema asilimia 80 (watu 3000) watachukua watu wa Dodoma kwa hiyo ni jambo kubwa sana. Hii ni fursa kubwa hata kipindi hiki cha ujenzi,”amesema.

Friday, 26 January 2018

Audio | Lava Lava – Tattoo | Mp3 Download

Audio | Lava Lava – Tattoo | Mp3 Download

Audio | Lava Lava – Tattoo | Mp3 Download

Audio | Foby – Ngangana | Mp3 Download

Audio | Foby – Ngangana | Mp3 Download

Audio | Foby – Ngangana | Mp3 Download

Rais Trump aombwa kuchukua choo cha dhahabu


 
Choo cha dhahabu alichopendekezewa rais Donald Trump
Jumba la kumbukumbu la Guggenheim mjini New York limekataa ombi kutoka kwa rais Donald Trump la kutaka kupewa mchoro wa msanii Van Gogh ili kuwekwa katika ikulu ya Whitehouse kulingana na vyombo vya habari.

Jumba hilo liliomba msamaha kwa kutoweza kupeana picha hiyo na badala yake likaomba kumpatia rais Trump choo cha dhahabu kulingana na gazeti la The Washington Post.

Lakini jumba hilo la kumbukumbu lilipendekeza limpatie rais Trump kiti hicho cha choo chenye dhahabu karati 18.

Ikulu ya Whitehouse haijatoa tamko lolote.

Kulingana na gazeti hilo,mhifadhi wa vitu katika jumba hiloi Nancy Spector aliojibu ombi hilo la Ikulu mwezi Septemba.

''Naomba msamaha...kukujulisha kwamba hatuwezi kushiriki katika kukupatia picha hiyo kwa kuwa ni miongoni mwa mkusanyiko wa Thannhauser ambao hawaruhusiwi kutoka nje ijapokuwa kwa maswala yasio ya kawaida'', aliandika katika barua pepe.

Picha hiyo ya 1888 ya Van Gogh, barua hiyo iliongezea itaonyeshwa katika taasisi dada kutokana na ruhusa kutoka kwa wamiliki wake.

Hatahivyo , muhifadhi huyo ameongezea kwamba choo hicho cha dhahabu kilichotengezwa na msaani wa Itali Maurizio Cattelan kiko tayari kwenda Ikulu kwa ''mkopo wa muda mrefu''.

Ni jambo la kawaida kwa marais wa Marekani na wake zao kuomba kazi za usanii ili kupamba baadhi ya vyumba katika Ikulu ya Whitehouse.

Tambwe kuivaa Azam FC kesho?


Straika wa Yanga, Amissi Tambwe raia wa Burundi ameshindwa kufanya mazoezi ya pamoja na wenzake kutokana na majeraha ya goti.

Hali hiyo imekuja ikiwa ni siku chache tangu arejee na acheze mechi dhidi ya Mwadui FC kabla ya kuwavaa Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Katika mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar. Mshambuliaji huyo akiwa amekaa nje ya uwanja huku wenzake wakiendelea na mazoezi.

Mshambuliaji huyo, alipata majeraha hayo juzi Jumatano katika mazoezi ya timu hiyo baada ya kugongana na beki wa pembeni, Juma Abdul na kushindwa kuendelea na programu nyingine.

Kutokana na Tambwe kushindwa kufanya mazoezi ya mwishoni ikiwa ni siku moja kabla ya mchezo huo, upo uwezekano wa Mrundi huyo kuikosa mechi dhidi ya Azam FC.

Katika mazoezi hayo ya jana, benchi la ufundi la timu hilo, lilionekana kuwaandaa baadhi ya washambuliaji watakaocheza nafasi yake ambao ni Juma Mahadhi na Yohana Nkomola.



Rais Magufuli,Mama Janet wamchangia Wastara Fedha za matibabu




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mke wake Mama Janet Magufuli hii leo wamemchangia muigizaji wa filamu Tanzania Wastara Juma shilingi milioni 15, kumsaidia katika matibabu yake.

Fedha hizo ambazo Wastara amekabidhiwa na Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike , sambamba na kiasi kingine cha milioni moja na laki tisa ambayo ni michango kutoka kwa wasaidizi wa Rais.

Msanii huyo amekuwa akisumbuliwa na mguu kwa muda mrefu na alikuwa kaomba msaada wa watanzania mitandaoni ili aweze kwenda nchini India kupatiwa matibabu.

Rais Magufuli anakuwa mtu wa kwanza kutoa fedha nyingi kwa msanii huyo, tangu aanze kutoa rai ya kuomba michango, ambapo wiki iliyopita waziri wa Habari, sanaa, michezo na utamaduni Dkt. Harison Mwakyembe alimkabidhi shilingi milioni moja.
Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akimkabidhi fedha Wastara

Kesi ya Tido Mhando yaahirishwa hadi Februari 23


Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando amepata dhamana baada ya kukidhi masharti na kutakiwa kurejea Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Februari 23, mwaka huu.

Tido alifikishwa mahakamani hapo saa 5:22  asubuhi na aliingizwa katika ukumbi wa mahakama ya wazi kabla ya kusomewa mashtaka matano.

Leo Januari 26, mwaka 2018 wakili wa Takukuru, Leonard Swai amedai mbele ya hakimu mkazi mkuu wa makahama hiyo,  Victoria Nongwa kuwa Mhando anatuhumiwa kwa mashtaka matano.
Swai amesema Juni 16, 2008 katika maeneo ya Dubai, United Arab Emirates (UAE), Tido akiwa mwajiriwa wa TBC kama Mkurugenzi Mkuu kwa makusudi alitumia madaraka yake vibaya kwa kusaini mkataba wa makubaliano kwa ajili ya kuendesha na utangazaji wa vipindi vya televisheni kati ya TBC na Channel 2 group Corporation ( BV1) bila ya kupitisha zabuni kinyume  na sheria ya manunuzi na kuisababishia BVl kupata manufaa.

Shtaka la pili, Tido anadaiwa Juni 20, 2008  katika maeneo ya utekelezaji wa kazi yake alitumia madaraka vibaya kwa kusaini makubaliano (wakuu wa makubaliano) kwa utangazaji wa digital duniani kati ya TBC na BVl.

Shtaka la tatu, Agosti 11, 2008  na Septemba 2008 katika maeneo hayo, Tido anadaiwa kutumia  vibaya madaraka yake kwa kusaini mkataba wa makubaliano (kuongeza wakuu wa mkataba ) kwa ununuzi, usambazaji kufunga vifaa vya usambazaji na mnara wa utangazaji kati ya TBC na BVI na kuisababishia BVI kupata faida.

Shtaka la nne, Tido anadaiwa Novemba 16,2008 akiwa Dubai, United Arab Emirates alitumia vibaya madaraka yake kwa kusini mkataba wa makubaliano (kuongeza wakuu wa mkataba ) kwa kuendesha miundombinu ya utangazaji (DTT broadcast infrastructure) kati ya TBC na BVI na kusababisha BVI kupata manufaa.

Katika shtaka la tano, Tido anadaiwa kati ya Juni 16 na Novemba 16, 2008 katika maeneo hayo ya United Arab Emirates aliisababishia hasara TBC ya Sh 887, 122,219.19.
Baada ya kusomewa mashtaka hayo, Tido ambaye anatetewa na wakili Ramadhani Maleta alikana mashtaka yote.

Swai alidai mahakamani hapo kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.
Hakimu Nongwa alimtaka mshtakiwa kutoa fedha taslimu mahakamani hapo Sh444 milioni ama hati ya mali isiyohamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha.

Mbali na sharti hilo, pia awe na wadhamini wawili ambapo watasaini hati ya dhamana ya maneno yenye thamani ya Sh500 milioni na asitoke nje ya nchi bila ya kuwa na kibali cha mahakama.
Mshtakiwa alikamilisha masharti hayo kwa kuwasilisha hati za mali na wadhamini wawili nyakati za saa sita mchana na kuondoka.

Kesi imeahirishwa hadi Februari 23, 2018 kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali (PH).
Kuhusu dhamana hiyo, DPP alipeleka hati ambayo inaipa mamlaka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuisikiliza kesi hiyo.

Mhando ni miongoni mwa waandishi wa habari na watangazaji mahiri na wakongwe ndani na nje ya nchi ambaye amewahi kufanya kazi Shirika la Utangazaji Uingereza (BBC).
Pia amewahi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) inayochapisha magazeti ya Mwananchi, Mwanspoti na The Citizen na sasa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media.

Nyumba za Askari Magereza zatakiwa kukamilika ndani ya miezi mitano


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali mstaafu, Projest Rwegasira ametoa miezi mitano kwa Wakala wa Majengo (TBA) kukamilisha ujenzi wa nyumba za askari wa Jeshi la Magereza zilizoko Ukonga jijini Dar es Salaam.

Ametoa agizo hilo leo Ijumaa Januari 26,2018 alipofanya mazungumzi na maofisa wa TBA na wa Jeshi la Magereza baada ya kukagua ujenzi huo.

“…fanyeni juu chini mhakikishe mradi huu unakamilika ndani ya miezi hiyo mitano mliyosema. Ongezeni nguvu ili mkamilishe mradi huu kwa wakati,” amesema katika taarifa iliyotolewa na wizara.

Fedha za ujenzi wa nyumba hizo unaogharimu  Sh10 bilioni zilitolewa na Rais John Magufuli baada ya kufanya ziara Ukonga mwishoni mwa mwaka 2016.

Soma: Waziri Mkuu aagiza wakala wa majengo Mara kukamatwa

Ujenzi ulianza mwaka jana badala ya Desemba 19, 2016.